Habari za Punde

ZAECA yawafikisha mahakamani watu 14 kwa makosa ya rushwa na uhujumu uchumi

 

Mamlaka ya kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) kwa kushirikiana na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Tarehe 29/12/2022 imewafikisha Mahakama Kuu Tunguu-Zanzibar Watuhumiwa Kumi na Nne (14) kwa makosa mbali mbali ya Rushwa na Uhujumu Uchumi kinyume na Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

Watuhumiwa hao pamoja na Kesi zao ni:-

1.    KESI NAMBARI 126/2022

WATUHUMIWA

1. KASSIM JUMA KHAMIS (52) mkaazi wa TOMONDO-Zanzibar aliyekuwa Mshika Fedha Mkuu wa Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU)

2. MACHANO KOMBO KHAMIS (42) mkaazi wa KIJICHI -Zanzibar aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU)

 3. ALI OTHMAN YUSSUF (43) mkaazi wa Mjini-Zanzibar aliyekuwa mwingiza taarifa kwenye mfumo wa malipo Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU)

4. KHAMIS ALI KHAMIS (37) Mkaazi wa CHUKWANI -Zanzibar aliyekuwa Msimamizi wa Mfumo wa Malipo (System Administrator) wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar 

Watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa kosa la:- Ubadhirifu wa Mali na Mapato Tsh. 314,307,950/- kinyume na Kifungu cha 42(2) (b) cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

Kesi imesomwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu Mh. Rabia Hussein Mohamed ambapo Watuhumiwa hao wamekana makosa yao na wamepewa dhamana ya Bondi ya Tsh. 20,000,000/= kila mmoja pamoja na wadhamini wao. Isipokuwa Mtuhumiwa KASSIM JUMA KHAMIS ambae amenyimwa dhamana yake.

Kesi hii itatajwa tena 10/01/2023 kwa ajili ya uamuzi mdogo.

 2. KESI NAMBARI 129/2022 WATUHUMIWA

 1. ALI KHAMIS ALI (43) mkaazi wa MAMBOSASA-Zanzibar aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.

2. KHAIRAT G. SANGA (38) mkaazi wa FUONI-Zanzibar aliyekuwa Msaidizi Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.

 3. FATMA ABDALLA HASSAN (42) mkaazi wa MWERA-Zanzibar aliyekuwa Msaidizi Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.

4. TALIB ABDULMANAN AMEIR (50) mkaazi wa KAMA-Zanzibar aliyekuwa Mshika Fedha Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.

 5. KHAMIS ALI KHAMIS (37) Mkaazi wa CHUKWANI -Zanzibar aliyekuwa Msimamizi wa Mfumo wa Malipo (System Administrator) wa Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar

 Watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa makosa ya :-

 1. Ubadhirifu wa Mali na Mapato kinyume na Kifungu cha 42(2) (b) cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

2. Kutumia vibaya Mali kinyume na Kifungu cha 43 cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

3. Matumizi Mabaya ya Ofisi kinyume na Kifungu cha 53 cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

Watuhumiwa hao kati ya mwaka 2014 na 2015 kwa makusudi waliuchezea Mfumo wa Malipo wa Serikali “EPICO 7” na kujipatia bila ya halali jumla ya Tsh. 81,940,228/- na kusababisha hasara kwa Serikali.

Kesi hii imesomwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu Mh. Rabia Hussein Muhamed ambapo Watuhumiwa wamekana makosa yao na wamenyimwa dhamana hadi terehe 10/01/2023 kwa ajili ya uamuzi mdogo.

3. KESI NAMBARI 127/2022 WATUHUMIWA

1. KHATIB ALI HAMDU (48) mkaazi wa CHUKWANI-Zanzibar aliyekuwa Mhasibu Mkuu Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM).

 2. MUHAMMED MAKAME ALI (40) mkaazi wa SHARIFUMSA Zanzibar aliyekuwa Muingizaji taarifa kwenye Mfumo wa Malipo Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM).

3. KHERI ALI ABDALLA (41) mkaazi wa FUONI -Zanzibar aliyekuwa Mtunza Ghala Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM) Watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa makosa:-

 1. Matumizi Mabaya ya Ofisi kinyume na Kifungu cha 53 cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

2. Ubadhirifu wa Mali na Mapato Tsh. 20,000,000/- kinyume na Kifungu cha 42(2) (b) cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

Kesi hii imesomwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu Mh. Rabia Hussein Mohamed ambapo Watuhumiwa hao wamekana makosa yao na wamepewa dhamana ya Bondi ya TSh. 20,000,000/- kila mmoja na wadhamini wao wawili TSh. 10,000,000/- kila mmoja.

 Kesi hii itatajwa tena 10/01/2023 kwa ajili ya uamuzi mdogo.

 4. KESI NAMBARI 128/2023 WATUHUMIWA

 1. MSANIFU SHAKA JUMA (39) mkaazi wa Mjini -Zanzibar

 2. MOHAMMED MWALIMU PONGWA (28) mkaazi wa SHAKANI-Zanzibar wote ni Watumishi wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) kwa nafasi ya Wauzaji umeme katika Kituo cha kuuzia umeme Makunduchi. Watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa makosa ya:-

 1. Matumizi Mabaya ya Ofisi kinyume na Kifungu cha 53 na 61 cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

2. Ubadhirifu wa Mali na Mapato kinyume na kifungu cha 42(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012.

Watuhumiwa hao bila ya halali walijipatia Tsh. 142,992,909/- kwa kutowasilisha fedha hizo Benki baada ya mauzo ya umeme katika kituo cha Makunduchi. Kesi hii imesomwa mbele ya Jaji wa Mahakama Kuu Mh. Mohamed Ali Mohamed ambapo Watuhumiwa hao wamekana makosa yao na wamepewa dhamana kila mmoja na wadhamini wao wawili bondi ya TSh. 50,000,000/- Kesi hii itatajwa tena 06/01/2023 kwa ajili ya kuwasilisha maelezo ya mashahidi.

 5. KESI NAMBARI 125/2022 MTUHUMIWA

1. SHEHE ALI SHEHE (41) mkaazi wa TOMONDO -Zanzibar Mfanyakazi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Zanzibar.

Mtuhumiwa anashtakiwa kwa kosa la :- Kuomba na kupokea Rushwa ya Tsh. 650,000/= pamoja na Matumizi Mabaya ya Ofisi kinyume na Kifungu cha 53, 36(3)(a) na 61 cha Sheria ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar, nambari 1 ya mwaka 2012. Kesi hii imesomwa mbele ya Jaji wa Mahkama Kuu Mh. Mohamed Ali Mohamed ambapo Mtuhumiwa amekana kosa lake na amepewa dhamana ya bondi ya Tsh. 500,000/= na wadhamini wawili.

Kesi hii itatajwa tena 06/01/2023 kwa ajili ya kuwasilisha maelezo ya mashahidi.

IMETOLEWA NA: Kitengo cha Uhusiano, Mamlaka ya kuzuia rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar (ZAECA

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.