Habari za Punde

Tatizo la Uharibifu wa Mazingira Zanzibar Sio Jambo Lililoanza Mara Moja -Mhe Othman

Na.Rashid Omar  OMKR.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanibar  Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba tatizo la uharibifu wa mazingira Zanzibar  sio jambo lililoanza mara  moja,  bali limetokea pole pole hadi kuweza kusababisha athari kubwa katika maeneo mbali mbali ikiwemo uharibifu mkubwa  wa vyanzo vya maj nchini.

Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipozungunza  na Viongozi wa Taasisi za Dini na Jumuiya zisizo za Serikali kuelezea mpango wa Serikali wa Kuirithisha Zanzibar kuwa ya kijani ambapo mpango huo wa kitaifa unatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.

Mhe. Makamu amesema kutokana na hali hiyo  hivi sasa uzalishaji wa maji safi na salama umeshuka sana kutokana na vyanzo vingi vya maji kuharibika na vyengine kukauka  jamblo linalotaokana na wananchi kuendelea kujenga taibia ya uharibifu wa mazingira ikiwemo ukataji wa miti ovyo.

Mhe. Makamu amefahamisha kwamba kutokana na hali hiyo serikali imekuja na mpngo wenye mikakati shirikishi itakayosaidia kubadili tabia za wananchi wa Zanzibar na kujajengea  utamaduni mpya kwa  watoto wote kupenda na kuheshimu miti sambamba na kufahamu thamani ya kila miti nchini katika kuendeleza maisha bora ya  wananchi.

Aidha emesema kwamba ukataji wa miti na uharibifu wa maizingira pia hivi sasa umechangia  kuwepo kasi kubwa ya maji ya bahari kuvamia makaazi ya wananchi  sambamba na kuwepo mvua  zisizotabirika huku hali ya joto  ikongezeka na kuathiri maisha ya watu katika maeneo mbali mbali.

Mhe. Othman amefahamisha mpango huo wa serikali ambao tayari umepata Baraka katika ngazi zote za serikali unakusudia kuwa jumuishi katika  utekelezaji wake utakaowashirikisha wadau mbali mbali wakiwemo watendaji wa taasisi za serikali, NGO’s pamoja na Taasisi za dini wakiwemo wananchi wa kawaida.

Amefahamisha kwamba matumaini ya serikali katika utekelezaji wa mpango huo kuwajengea utamaduni mpya wananchihasa  vijana  kutambua thamani ya kuirithisha na kuiweka Zanzibar kuwa ya kijani ili kuifanya nchi kutokuwa na athari kubwa inayotokana na  uchafuzi wa manzingira kutokana na shughuli za kibinaadamu.

Amesema kwamba  kwa mujibu wa matokeo ya sensa ya mwaka 2022 Zanzibar inaongezeko la watu takribani  laki sita, ikilinganishwa na sensa ya mwaka 2012, huku eneo lote la ardhi ya Zanzibar likeendelea kuwa hekta  za mraba  elfu mbili na mia sita  tu ambazo zinaendelea kupungua kutokana na changamoto ya maji ya bahari kuvamia ardhi.

Mhe. Othman ameongeza kwamba Jumuiya na taasiisi mbali ni vyema  kushirikiana na wananchi wote  katika kuunga mkono juhudi hizo malum  kwa kushiriki katika harakati mbali mbali ikwemo upandaji wa  miti  katika maeneo tofauti ikiwemo ya mikoko  kuitunza na kudhibiti ukataji ovyo wa miti ya aina zote nchini.

Mhe. Othman amesema pamoja na mambo mengine katika utekelezaji wa mpango huo serikali kwa kushirikiana na wadau mbali mbali itatoa elimu kwa wananchi sambamba na kushughulikia uzalishaji wa miche ya miti mbali mbali pamoja na ushajiishaji wa wadau katika kuhamasisha juu ya ushiriki wa kila mmoja katika kutekeleza mpango huo sambamba na kutoa tunzo kwa kikundi , mtu ama taasisi zitakazofanya vyema zaidi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hya Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Zanzibar (ZEMA) ndugu Sheha Mjaja  Juma amesema kwamba katika utekelezaji wa mpango huo serikali inakusudia kupanda miti ya aina mbali mbali zaidi ya milioni tatu kila mwaka.

Amfahamisha kwamba miti hiyo itaoteshwa katika maeneo mbali mbali ya visiwa vya Unguja na Pemba kwa kupitia ushiriki wa wadau mbali mbali wakiwemo wanafunzi, Jumiya za Kirai  chini ya usimamizi wa Kamati maalum ya serikali kuu ili kuhakikisha kwamba Zanzibar inarejeshewa hadhi ya uoto wa asili ya kijani.

Mapema viongozi hao wa NGO na taasisi za Dini walimueleza Mhe. Makamu kwamba taasisi zao zipo tayari kushirikiana na serikali katika utekelezaji wa mpango huo hasa katika suala la kutafuta shughuli mbadala za kiuchumi kwa wananchi katika kuondokana na suala la ukataji wa miti ovyo.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha habari leo tarehe 28.04.2023.

   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.