Habari za Punde

Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) Lakabidhi Zawadi ya Bodaboda kwa Wakala Bora kwa Mwezi wa Aprili 2023

Meneja wa Shirika la Bina Zanzibar Kanda ya Ziwa Ndg. Bahatisha Suleiman akimkabidhi zawadi ya Pikipiki mshindi  Wakala wa Sunshine Insurance Agency katika kuthamini mchango wake katika ukuaji wa Biashara kwa Shirika hilo hususan kwa Mwezi Aprili, 2023.


Na. Mwandishi Wetu Mwanza. 

Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) limetoa zawadi ya Piki piki kwa wakala wake Sunshine Insurance Agency kama njia ya kuthamini mchango wake na jitihada alioonesha katika mwezi wa Aprili, 2023.

(ZIC)limemzawadia Piki piki aina ya TVS 125 wakala wake aitwae Sunshine Insurance Agency katika kuthamini mchango mchango wake katika ukuaji wa Biashara kwa Shirika hilo hususan kwa Mwezi Aprili, 2023.

Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) linatarajia kuadhimisha miaka 54 katika biashara ya bima ifikapo tarehe 20 ya mwezi Juni, 2023. Katika kuhakikisha wanaendelea kuwanyanyua mawakala wao kwa kuwapatia vitendea kazi mbali mbali, Shirika limekuja na mpango wa kutoa pikipiki kwa kila wakala ambae atafanya vizuri zaidi katika kila mwezi.

Katika hafla ya kukabidhi pikipiki hiyo kwa Sunshine Insurance Agency, Meneja wa Kanda ya Ziwa Ndg. Bahatisha Suleiman amewapongeza washindi hao kwani jitihada zao binafsi ndiyo zilizopelekea kushinda zawadi hiyo.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Shirika la Bima la Zanzibar Ndg. Mohamed Shaaban amesema zawadi hii itakwenda kuwa chachu ya jitihada kwa mawakala wengine ambao nao wana nafasi ya kujishindia pikipiki katika miezi ijayo.

Aidha, Uongozi wa Sunshine Insurance Agency kupitia Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Ndg. Happiness Lyatuu Mkelemi wametoa shukurani zao za dhati kwa kupatiwa zawadi hiyo na wameahidi kuendelea kuwahudumia wateja wa Shirika la Bima la Zanzibar kama dira na mikakati ya Shirika hilo inavyoelekeza.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.