Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Mwinyi Amewatembelea Wazee Kwa Kuwasalimia na Kuwajulia Hali Zao

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kumjulia hali yake Msanii Maarufu wa Zanzibar Bi.Mwapombe Hiyari, alipofika nyumbani kwake Chuini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja leo 23-2-2024, ikiwa ni utaratibu wake kuwajulia hali Wazee mbalimbali Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Familia ya Mzee Daudi Suleiman Ali, , kuitikia dua, alipofika nyumbani kwake Fuoni Wilaya ya Magharibi “B” Unguja kwa ajili ya kumsalimia na kumjulia hali yake leo 23-2-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na Mzee Ramadhan Nzori , aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Jangombe Zanzibar, alipofika nyumbani kwake Jangombe Wilaya ya Mjini Unguja kwa ajili ya mazungumzo na kumjulia hali yake leo 23-2-2024

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.