Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ameutaka uongozi Zanzibar SUKUK kupitia PBZ kufanya jitihada zaidi za kutoa elimu kwa umma kuhusu huduma
za SUKUK kupitia Benki hiyo ili kusaidia kuukabili ushindani mkubwa uliopo katika
biashara ya fedha hapa nchini.
Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini
kwake migombani mjini Zanzibar alipokutana na ujumbe wa PBZ uliofika kwa mazungunzo
kuhusiana na mradi wa uwekezaji wa SUKUK kupitia Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ
IKHILAS.
Amefahamisha ili kupata ufanisi
kupitia huduma za BPZ IKHILAS kunahitajika kujengwa uelewa mkubwa kwa jamii
hivi sasa katika kuendesha na kusimamia biashara za fedha na uwekezaji wa aina hiyo sambamba na kujitahidi kujenga uwezo kwa
watendaji mbali mbali walionao katika
kukabili biashara kwa mbinu za kisasa zaidi.
Amesema kwamba kuna haja kubwa
benki ya PBZ kuyatumia majukwaa ya
kidijitali kujitahidi kuwafikia wananchi waliowengi zaidi ambao ndio wateja na
wateja watarajiwa wa huduma za benki hiyo kwa uwekezaji miradi kama ya SUKUK
ikiwemo huduma za mikopo na nyenginezo zinayoanzishwa ndani ya benki hiyo kupitia PBZ Ikhilas
inayozingatia misingi ya uislamu.
Amesema katika kipindi hiki chenye
ushindani mkubwa wa kibiasara za fedha ni vyema watendaji na viongozi wa Benk hiyo
kuwa wabunifu zaidi na kutumia maarifa na elimu kuchangia maendeleo makubwa ya
Benki hiyo ambayo ni miongoni mwa benki kongwe nchini Tanzania.
Amesema kwamba Zanzibar zipo fedha
nyingi kutoka mikononi mwa wananchi
zinazoweza kuwekezwa lakini azijafanyiwa ivyo kutokana na sababu zao
mbali mbali za kidini walizonazo wananchi na kwamba elimu ni jambo pekee
linaloweza kubadili mazingira na
mwelekeo wa namna hiyo kwa jamii.
Hata hivyo, Mhe. Makamu amesema
kwamba huduma za PBZ IKHILAS zinaitajika sana ndani ya jamii ya Zanzibar katika
kubadili mfumo wa kiuchumi wa wanajamii uliozoeleka hapa Zanzibar iwapo watakuwa na elimu ya kutosha.
Aidha amewataka ujumbe huo kujaribu
kuainisha uwezo na changamoto na matatizo mbali mbali waliyonayo yanayohitaji ufumbuzi wa serikali kuu
kuyawasilisha pamoja na mapndekezo yake ili yatatauliwe.
Naye Mkurugenzi wa PBZ Ikhlas Rajab
Mohammed Ramia aliyeongoza ujumbe huo, amesema kwamba Mradi wa Zanzibar SUKUK
unalengo la kukuza uwekezaji katika biashara
ya fedha na huduma za kijamii kwa misingi ya uislamu.
Amesema kwamba huduma za uwekezaji
wa skuk imeazna kutolewa hapa Zanzibar kupitia PBZ IKHILAS kwa takribani miaka mitano iliyopita kwa taasisi
za watu binafsi ambazo zimefanikiwa sana katika mwelekeo wa kukuza Mipango ya
Benki ya kiislamu.
Amesema kwamba
Mwisho
Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo cha habari leo jumanne Machi 26, 2025.
No comments:
Post a Comment