Na Fatma Kassim, Maelezo
BODI ya Chakula Dawa na Vipodozi Zanzibar
imerejesha ilikotoka Pakistani mchele tani 245 aina ya Alminara, baada ya
kubainika kuwa haufai kwa matumizi ya mwanadamu.
Mchele huo ulioingizwa nchini mapema
mwezi uliopita, ulikuwa tani 260 ambapo baada kuruhusiwa kwa makontena saba na
wafanykazi wasiowaaminifu wa Bodi hiyo waliopo Bandarini na ulisababisha kufika
masokoni na kusababisha kupungua kwa tani 14.
Mkaguzi wa Chakula wa Bodi hiyo, Khamis
Ali Omar, alisema zoezi zima la kukusanya mchele huo umefanywa na Bodi hiyo na
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na mwenye mali hiyo lilifanyika mara baada ya
kuonekana mchele huo haufai kwa matumizi ya mwanadamu.
Alifahamisha kuwa hivi sasa Bodi
inafanya kila jitihada ya kuusaka mchele huo katika maduka na wakifanikiwa
kuuona watahakikisha unaangamizwa ili usiweze kuathiri watumiaji wa mchele huo.
Amewataka wananchi wakiuona mchele huo
ama bidhaa yoyote ambayo wataitilia shaka kutoa taarifa kwa bodi hiyo ili
kuweze kuchukuliwa hatua zinazofaa ikiwemo kufanyika kwa uchunguzi ili zisiweze
kuleta athari kwa wananchi.
Kwa upande wa mfanyabiashara huyo
Mohammed Mauliy ameishukuru Serikali kwa kuweza kumpatia kibali ambacho
kitamuwezesha kurejeshewa gharama zamchele wake huo.
Aidha ameilaumu kampuni MSC
iliyomsafirishia mchele huo kutoka Pakistani kwa kumsababishia hasara kubwa
ikiwa ni pamoja na mpaka sasa kutumia karibu milioni 60 kwa usafirishaji tu na
kuwataka wafanyabiashara wengine wasitumie kampuni hiyo.
Alifahamisha kuwa kutokana na gharama
kubwa zitokazotumika kwa kusafirishia hapa Zanzibar watausafirisha mchele huo
hadi Mombasa kwa tajiri mwenyewe na baadae kufanya utaratibu wa kuusafirisha
kuelekea Pakistan.
No comments:
Post a Comment