Kwa kuamua kujiuzulu bila ya kuwashauri
Na Abdi Suleiman, Pemba
Aliyekuwa Waziri wa Miundo mbinu na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambae pia ni mwakilishi wa
jimbo la Ole, wilaya ya Wete Mkoa wa kaskazini Pemba, Hamad Massoud Hamad, amewaomba
radhi wapiga kura wake, wa jimbo la Ole kwa uamuzi wake wa kujiuzulu bila ya
kuwashauri.
Mwakilishi huyo, aliyasema hayo jana huko
Maambani Ole, wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa jimbo la Ole, kwa mara
ya kwanza baada ya kujiuzulu wadhifa huo.
Hamad Massoud alisema kuwa, uamuzi
aliouchukuwa wa kuamua kujiuzulu kwake ni sahihi na wa kishujaa, na alifanya
hivyo baada ya kuwashauri viongozi wake wakuu wa chama chake, na ndipo
alipomuandikia barua Rais wa Zanzibar .
“Nimefanya kitendo bila ya kuja kuwashauri
sio kwa sababu ya ujeuri, sio najua sana mimi ni mwakilishi na uwaziri, katika
kitu ninacho kiheshimu ni heshima nilioyopewa na watu wa ole ambao ndio
nyinyi” Alieleza Mwakilishi Hamad Massoud.
“katika siasa za Zanzibar Ole ndiko kwenye
chuo cha siasa, kwasababu ya umoja na ukarimu wa watu wa Ole, na ndio
waliomuweka madarakani kwa kura 5564 sawa na asilimia 86 niliteuliwa kuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano”alifahamisha Hamad.
Alieleza kuwa baada ya kutafakari Julai 20 aliamua kumuandikia barua Rais ya kujiuzulu kwake, baada ya kushauriana na viongozi
wenzake wa CUF, na Rais kuliridhia ombi la kujiuzulu kwake.
Aidha aliwataka wananchi wasisikitike wala
kuhuzunika kutokana na na uamuzi wake aliouchukuwa, na kuwaomba wamuunge
mkono kufuatia uamuzi wake aliouchukua.
Kwa upande wao wananchi wa jimbo hilo la Ole, wamesema
kuwa, kujiuzulu kwake ni moja ya kuonyesha ukokamavu wa kisiasa sambamba na
kukijengea heshima chama chao cha wananchi CUF.
Wananchi hao walifahamisha kuwa, Mwakilishi
wao, ni muda mfupi tokea kuchaguliwa kwake lakini mafanikio makubwa yamepatikana katika Wizara ya Miundo mbinu na Mawasiliano hususan suala la ujenzi wa barabara
na Uwanja wa Ndege wa Zanzibar .
“Kujiuzulu, kumeleta faraja kubwa kwake na kwa taifa nzima kwani ni kaonyesha ujasiri wa kukomaa kisiasa na
kisaikolojia, sambamba na kukijengea sifa chama chetu cha Cuf” walifahamisha
wananchi hao.
Walifahamisha kuwa kujiuzulu kwa Mwakilishi
huyo, ni heshima kubwa kwa serikali yao
ya umoja wa kitaifa, kwani tayari wako baadhi ya viongozi wanatuhumiwa kwa
kuiba mamilioni ya shilingi, huku wakishindwa kujiuzulu.
Naye mwenyekiti wa CUF wilaya ya Wete,
Khalfan Moh’d Issa, amesema kuwa, kujiuzulu kwa Hamad Massoud ndio utamaduni wa
chama chao, kwa viongozi kusamehe maslahi yao binafsi kwa lengo la kuijengea
hashima Serikali ya Zanzibar.
Mwenyekiti huyo, alisema kuwa Zanzibar imefika wakati kwa viongozi wake watakaobainika
na kashafa ya aina yoyote kuweza kujiuuzulu, ili kuepuka kuitia aibu serekali yao .
Naye aliyekuwa Mwakilishi wa jimbo la
Chambani Abassi Juma Muhunzi, aliwataka wananchi wa Ole kumuunga mkono
mwakilishi wao, kwani kufanya hivyo ni kumekijengea heshima kubwa chama chao na
kuonyesha ujasiri wa kisiasa.
Muhunzi alisema kuwa, kitendo alicho
kifanya Hamad Massoud ni kitendo cha kishujaa, na kitu ambacho hakijawahi
kutokea tokea mwaka 1964, hivyo kiwe mfano kwa viongozi wa Zanzibar,
watanzania na Afrika mashariki na kati ambapo utamaduni huo haupo.
No comments:
Post a Comment