Habari za Punde

Dk Shein afanya uteuzi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amemteuwa Mussa Msheba Suleiman kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Usafiri wa Barabarani katika Wizara ya Miundo Mbinu na Mawasiliano,Zanzibar.
Kwa mujibu wa Taarifa iliotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt Abdulhamid Yahya Mzee imeeleza kuwa Rais amefanya uteuzi huo kwa mujibu ya uwezo aliopewa chini ya kifungu Namba 14((2)(a) cha sheria ya Usafiri wa Barabarani(THE ROAD TRANSPORT ACT)Namba 7 ya mwaka 2003.
Uteuzi huo umeanza tarehe 6 Januarri, 2013.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIOBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.