Na Mwandishi wetu
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Madini na
Nishati, Eliakim Maswi, amekanusha tuhuma za Shirika la Umeme (TANESCO) kwamba
linaidai Zanzibar
kiasi cha shilingi bilioni 47 kutokana na matumizi ya umeme.
Alisema wamekuwa wakipokea shilingi
milioni 500 kila mwezi kutoka Shirika la Umeme Zanzibar, ikiwa ni malipo ya
umeme unaotumiwa Zanzibar .
Maswi alilazimika kutoa ufafanuzi huo
baada ya kuwasilisha mada kwa Wahariri na waandishi wa habari kuhusu mikakati inayochukuliwa
kuhakikisha kunakuwa na uhakika wa umeme utakaokidhi matakwa ya Mradi wa Matokeo
Makubwa Sasa (BRN) unaotazamiwa kuanza kutekelezwa mapema mwezi ujao hadi mwaka
2033.
“Kwanza niwaambie (waandishi wa
habari),deni hili ni la zamani sana ila ,SMZ imekuwa ikilipa kila mwezi na hata
hivi sasa tumepokea shilingi milioni 500
za malipo ya umeme kwa Zanzibar tu,” alisema.
“Nawaambia mkawaambie wote wanaosema kwamba
Zanzibar inadaiwa na TANESCO kuwa huo ni uongo na kama mtu hajafanya utafiti
hana haki ya kuzungumza,” alisema.
Pia,aliwataka wananchi kutowasikiliza
watu aliodai kuwa ni wanafiki kutokana na kuamua kuzungumzia mambo ya TANESCO nje bunge.
Aliwataka wanasisasa wanaosema kuhusu nishati na madini kuhakikisha
hawapotoshi ukweli.
Aidha alisema TANESCO na Wizara ya Madini na Nishati, zimekubaliana kutekeleza
mipango waliyojipangia ikiwa ni pamoja na kuhakikisha umeme unapatikana kwa
uhakika na kwa bei nafuu ili ifikapo 2025 na asilimia 75 ya Watanzania wawe wanatumia nishati hiyo.
Alisema,Juni 30 mwaka huu,wataipatia TANESCO shilingi bililioni 80 ikiwa ni ruzuku
kuhakikisha inapata uwezo wa kujiendesha.
No comments:
Post a Comment