Na
Said Ameir, Comoro
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, yuko
Comoro kuanza ziara ya kikazi ya siku nne kufuatia mwaliko wa Rais wa visiwa
hivyo, Mhe. Ikililou Dhoinine.
Katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa Prince Said Ibrahim mjini Moroni, Dk. Shein
alipokelewa na mamia ya wananchi wa mji wa Moroni na viongozi wa serikali
wakiongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Comoro, Mhe.Mohamed Ali Soilihi
pamoja na Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Chabaka Kilumanga.
Mara
baada ya kuwasili alikaribishwa kwa kupigiwa wimbo wa taifa na kuvishwa shada
la maua kulingana na utamaduni wa watu wa Comoro baadae kusalimiana na viongozi
wa serikali na kidini waliofika kumlaki.
Katika
mazungumzo mafupi uwanjani hapo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Comoro,viongozi
hao wawili walieleza haja ya kuimarisha ushirikiano wa kindugu na wa damu
uliopo kati ya Comoro na Zanzibar.
Alimueleza
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Comoro kuwa ziara yake itasaidia kuimarisha
uhusiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kufungua milango zaidi ya
ushirikiano kati ya nchi hiyo na Zanzibar.
Kabla
ya kuondoka kwenda Moroni, Dk. Shein alikagua vikundi vya sanaa na utamaduni na
kusalimiana na wananchi wengine walioshiriki mapokezi yake.
Jana
jioni atakutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Comoro, Ikililou
Dhoinine.
Mazungumzo
hayo yalikuwa juu ya kukuza uhusiano kati ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Comoro na pia kuimarisha ushirikiano kati ya Zanzibar na nchi hiyo.
Katika
ziara hiyo, Dk. Shein amefuatana na mke wake, mama Mwanamwema, Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora, Mhe. Dk. Mwinyihaji Makame Mwadini, Naibu
wa Waziri wa Kilimo na Maliasili, Mhe. Mtumwa Kheir Mbarak na Mshauri wa Rais
Ushirikiano wa Kimataifa, Uwezeshaji na Uchumi, Mhe.
Balozi Mohamed Ramia
Abdiwawa.
Wengine
ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Khamis Haji, Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Utamaduni, Utalii na Michezo, Ali Saleh Mwinyikai, Katibu Mkuu Wizara ya
Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto, Asha Ali Abdulla na
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Zanzibar,Kombo
Abdulhamid Khamis.
No comments:
Post a Comment