Habari za Punde

Watuhumiwa wengine escrow waburuzwa mahakamani

Na Mwandishi Wetu
Watuhumiwa wengine watatu waliokwapua fedha za escrow wamefikishwa katika kizimba cha mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu mashtaka ya kupokea rushwa.

Walioshtakiwa ni Mkurugenzi wa fedha wa benki ya Mkombozi, Julius Ruta, ambae amakosa dhamana, Ofisa Mwandamizi wa TANESCO, Steve Urasa na Leonard Lutabingwa wa TRA anayeshitakiwa kwa makosa manne.

Kushtakiwa kwa watendaji hao kunafanya idadi ya watu walioburuzwa mahakamani kutokana na sakata hilo kufikia watano.

Wengine ni  Rugonzibwa Mujunangoma na Theophillo Bwakea ambao walifikishwa mahakamai Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka ya rushwa baada ya kupokea mgao wa shilingi milioni 485.1 kutoka kwenye akaunti ya Tegeta Escrow walizohamishiwa na James Rugemalira.

Katika kesi ya kwanza, aliyekuwa Mwanasheria wa Mamlaka ya Vizazi na Vifo (Rita) Mujunangoma ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Sheria Wizara Ardhi, Nyumba Maendeleo ya Makazi, alisomewa mashitaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Emmilius Mchauru.


Upande wa Jamhuri ukiongozwa na Mwendesha Mashitaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai akisaidiana na Max Ari, ulidaiwa Februari 5, mwaka 2014 katika benki ya Mkombozi iliyopo Ilala jijini, mshtakiwa akiwa Mkuu wa Sheria wa wizara hiyo,alipokea rushwa.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa alipokea rushwa ya shilingi milioni 323.4 kama zawadi kupitia akaunti yake namba 00120102062001 kutoka kwa Mshauri binafsi wa kimataifa na Mkurugenzi wa zamani wa IPTL,James Rugemalira baada ya kuwa mjumbe katika menejimenti ya Rita wakati wa machakato wa kuipitisha IPTL kuiuzia Tanesco umeme.

Katika kesi ya pili, aliyekuwa mjumbe wa kitengo cha kuidhinisha Tanesco kununua umeme wa IPTL,Wizara ya Nishati na Madini, Injinia Bwakea kwa sasa mtumishi wa Wakala wa Umeme Vijijini(REA),alisomewa mashitaka yake mbele ya Hakimu, Frank Moshi.


Ilidaiwa mshtakiwa akiwa Injinia Mkuu wa REA, alipokea rushwa ya shilingi milioni 161.7 kupitia akaunti namba 00410102643901 ya Tegeta Escrow kama zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Rugemalira.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.