Na Mwandishi maalum
Wakati vuguvugu la uchaguzu
likikaribia na zikibaki ziku chache kabla ya
firimbi kupulizwa kuanza kampeni za uchaguzi ambao utafanyika hapo Okotba 25 kuna mengi yamejitokeza na ya kufurahisha ya kushtukiza pamoja na
mengine ya kushangaza. Viashiria vyote
hivyi vinaonesha uchaguzi wa mwaka huu unaweza ukaleta matokeo ya kushangaza
sana na yasiyotarajiwa
Moja katika mpambano wa kisiasa uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu
ulikuwa katika jimbo la Kiembesamaki ambapo Mwakilishi aliepo Mahmoud Thabit
Kombo ambaye ni naibu Waziri wa afya alitarajiwa atapambana na kukutana uso kwa
uso na Mwakilishi aliepoteza jimbo hilo baada ya kuvuliwa uanachama wa CCM, Mansour
Yussuf Himid.
Ulikuwa ni mpambano wa aina
yake kutokana na historia inayofanana ya vijana hawa wawili waliozaliwa na
kulelewa na wanamapinduzi. Mahmoud ni mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa muda mrefu
wa ASP Thabit Kombo Jecha na mwanamapinduzi, Mansour ni mtoto wa aliyekuwa
mwanamapinduzi brigerdier Yussuf Himid Mkuu
wa Kwanza wa Vikosi vya SMZ baada ya Mapinduzi ya mwaka 1964.
Mahmoud
na Mansour wote wamewahi kuwa mawaziri katika serikali ya Rais Amani Karume,
wajumbe wa NEC ya
CCM na wawakilishi wa majimbo ya Mpendae na Kiembesamaki kabla ya Mahmoud
kuhamia Kiembesamaki baada ya kufukuzwa uanachama wa CCM kutokana na kwenda
kinyume na maadili.
Kwa historia hii na mazingira ya jimbo la Kiembesamaki ambalo
CUF wameona uwezekano wa kulinyakua kupitia turufu ya Mansour wakati CCM
wakihakikisha linabaki katika mikono ya CCM kwa turufu ya Mahmoud.
Mpambano huu ulitarajiwa
utokee kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la kiembesamaki ila Mansour, sijui ni kwa
kushauriwa ua kwa kusoma alama za nyakati, hakupendekezwa na chama chake kipya
cha CUF alichojiunga kugombania uwakilishi wakati huu.
Mansour aliwahi kunukuliwa
akisema ikiwa
ataamua kurudi tena kwenye ulingo wa siasa atawania katika Jimbo la
Kiembesamaki ambako amewekeza na anadai anakubalika.
Wakati majina ya wagombea
uwakilishi yakisubiriwa kwa hamu hasa kwa jimbo la Kiembesamaki na CUF
kutangulia kutangaza majina ya wagombea 04/06/2015, Mansour alitajwa kwamba
atagombea jimbo la Kiembesamaki. Tulipowasubiri CCM kutangaza nao pia
walitangaza kwamba Mahmoud atagombea jimbo la kiembesamaki tarehe 13/08/2015. Tuliokuwa
tukisubiri mpambano huu tukaona sasa mambo yamewiva tutaweza kushuhudia tukio
la kihistoria kwenye kampeni na mpaka kwenye uchaguzi.
Wakati haya yakitokea Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ikatangaza majimbo mengine mane mapya na kuwa 54
badala ya 50 yaliyokuwepo. Moja katika jimbo jipya ni jimbo la Chukwani.
Ujio wa jimbo la Chukwani
ulifungua mlango mwengine ambao haukutarajiwa kwa vyama vyote viwili kwani ZEC
ilifanya siri kubwa kuyatangaza majimbo mapya na kuyaunganisha mengine kutokana
na jinsi ya mji unavyokuwa na watu kuhama na kuhamia sehemu nyengine. Pia CUF
walipotangulia kutaja majina ya wagombea kabla ya ZEC kutangaza majimbo
kumeleta sintofahamu kidogo ambayo inaweza kuwa ni neema pia.
Pengine CUF waliiona hii ni
fursa nzuri ya kujihakikishia kuepuka mpambano kati ya Mahmoud na Mansour
wakaamua kurusha taula kabla ya mpambano kuanza, kumuachia jimbo Mahmoud ambae
ninaamini amepata kupumua sana kwa kuwa angelikuwepo Mansour, ingebidi itumike
nguvu kubwa sana kwenye kampeni. Pia ni kama kula matapishi yake Mansour ambae
alituhakikishia kwamba akirudi kwenye siasa atagombea jimbo hili. Hivyo CUF
walipotangaza tena majina ya wagombea, Mansour atagombea jimbo la Chukwani
badala ya Kiembesamaki.
Ila kwa upande mwengine wa
shilingi, naamini huu ni mkakati ambao ninaweza kusema ni ‘bao la kisigino’
kwani Mansour kugombea jimbo jipya la Chukwani dhidi ya mgombea wa CCM, Mwanaasha Khamis Juma, uwezekano wa kulichukua CUF jimbo hili ni
mkubwa endapo CCM halitopiga ‘bao la mkono’ kama ilivyo kwa Mahmoud kushinda
jimbo la Kiembe Samaki dhidi ya mgombea wa CUF, Mohammed Nassor Mohammed pia
kwa ‘bao la kisigino’ na hatohitaji ‘bao la mkono’.
No comments:
Post a Comment