Habari za Punde

Mhe Said Soud na Juma Ali Khatib wateuliwa kuwa wajumbe wa Baraza la Mapinduzi


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalum:

i.            Mhe. Said Soud Said – Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum

ii.          Mhe. Juma Ali Khatib – Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum.
 
Uteuzi huo umeanza leo tarehe 9 Aprili 2016.
    
Waheshimiwa wote waliotajwa wanaombwa wafike Ikulu Mjini Zanzibar kesho Jumapili tarehe 10 Aprili 2016
saa 3 kamili za Asubuhi kwa ajili ya kuapishwa.



(Dkt. Abdulhamid Y. Mzee),
KATIBU WA BARAZA LA MAPINDUZI
NA KATIBU MKUU KIONGOZI,
ZANZIBAR.


                                                               
9 APRILI, 2016


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.