Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa TIB Corporate Bahati Minja (aliyesimama) akitoa ufafanuzi kuhusu huduma zinazotolewa na TIB Corporate Bank wakati wa mkutano wa Wakandarasi unaofanyika Jijini Mwanza
TIB
Corporate Bank imesema imekusudia kuwawezesha kifedha wakandarasi wa ndani ili
waweze kutekeleza vema majukumu yao ya kikandarasi.
Akizungumza
wakati wa mkutano wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi nchini (CRB) uliofanyika
jijini Mwanza, Mkuu wa Kitengo cha Mauzo ya Mikopo wa Benki ya TIB, Theresia
Soka amesema benki yake imekuja na suluhisho la kutatua changamoto za
wakandarasi wazawa.
TIB
Corporate Bank imemua kurahisisha taratibu zake za kutoa mikopo kwa wakandarasi
wa ndani kwa kuwataka kuwasilisha vielelezo tu vinavyomtambulisha kuwa
amesajiliwa kisheria ili aweze kupata mkopo.
‘Tumeamua
kurahisisha utaratibu wetu wa utoaji mikopo ili kuwawezesha wakandarasi na
hivyo kuchangia ukuaji wa maendeleo nchini katika sekta hii muhimu ya ujenzi’
alisema Bi Soka.
Naye
Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa TIB Corporate Bahati Minja, alisema
benki hiyo inayomilikiwa na Serikali, imeboresha huduma zake za kibenki ili
kuwawezesha wakandarasi wazawa.
‘Lengo
kubwa la Benki ya TIB Corporate ni kuhakikisha wakandarasi wanawezeshwa kifedha
ili wawe na vitendeakazi vya ujezi’ alisema Bi Soka.
Hata
hivyo wakandarasi waliohudhuria mkutano huo ambao miongoni mwao wamefadhiliwa
na benki hiyo, waliupongeza uongozi wa Benki ya TIB Corporate kwa kuamua
kuwawezesha kwa mikopo ya kikandarasi.
Wakandarasi
hao walisema uwezeshwaji huo wa mikopo nafuu inayotolewa na benki hiyo,
itawasaidia kuendesha kampuni zao za ujenzi kwa ufanisi zaidi.
Mkutano
huo wawakandarasi wenye kauli mbiu ya ‘Kuwajengea Uwezo Wakandarasi wa Ndani
kwa ajili ya Uchumi Endelevu', utafuatiwa na mkutano mwingine utakaofanyika
jijini Dar es salaam katika ukumbi wa Daimond Jubilee kuanzia tarehe 26 hadi 27
mwezi huu wa tano.
TIB
Corporate Bank imefanya mabadiliko ya kitaasisi ili kuweza kuwa kituo cha
huduma zote za kibenki kwa kushughulikia mahitaji ya wawekezaji wa ndani kwa
lengo la kusukuma maendeleo ya uchumi wa Taifa
No comments:
Post a Comment