Kampuni ya simu inayoongoza visiwani
Zanzibar,Zantel,mwishoni mwa wikii hii imefanikiwa kulinogesha tamasha la ‘Full
Moon Party’ linalofanyika kila mwezi visiwani Zanzibar na kufanikiwa kuvuta
mamia ya mashabiki.
Tamasha hilo maarufu linalojumuisha
burudani ya muziki na sarakasi, lilifanyika katika ufukwe wa Kendwa Rocks mkoa
wa Kaskizini Unguja likijumuisha burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali.
Kikundi cha Sarakasi cha Zanzibar
ndicho kilichoanza kutoa burudani kikifuatiwa na bendi ya FM Academia kutoka
Dar es Salaam, wakiongozwa na Nyoshi El Saadat, ambao waliacha gumzo kwa
burudani kali waliyoitoa.
Akizungumzia kuhusiana na tamasha hilo
Mkurugenzi Mtendaji wa Zantel, bwana Benoit Janin alisema lengo la Zantel
kudhamini tamasha hilo ni kukuza utalii wa ndani hapa nchini.
‘Tamasha hili linalenga kufungua
milango ya utalii nchini kwa kuonyesha vivutio vya kiburudani tulivyonavyo, na
hivyo kuiongezea mapato nchi yetu’ alisema bwana Janin.
Katika kunogesha zaidi tamasha hilo
Zantel ilimualika mtangazaji wa kipindi cha 5 Select cha East Africa TV, Tbway
kuwa mshereheshaji shughuli hiyo.
Tamasha la muziki Ramadhan hii, subhanah llaah, Zantel kwa hili tumewashtukia sasa mnakwenda against na maadili ya kiislam na kizanzibari, tunakwambieni tutahama Zantel na kuhamia mitandao mengine.
ReplyDeleteHii sio SubhanaALLAH bali ni Innalillahi wainna Ilayhi Raajiuun!! Kwani hiyo party ya full moon inafanyika katika siku ambazo ni sunna kufunga yaani mwenzi 13 14 15 katika kila mwezi!! Zanzibar imebakia jina tu! Halafu tunasema maisha magumu! Kwa mambo kama haya unafikiri itakuwje? Allaha atuhifadhi!! 1
ReplyDeleteHao Wapo kibiashara zaidi, ndugu yangu, na Zanzibar sio nchi ya kiislam,angalia mitaani, dhuluma na ufisadi n.k (Zanzibar wakaazi wake wengi ni waislam, hilo halina ubishi ila sio nchi yenye kufata sheria za kiislam).Laiti huyo Ali kilupi Angekuwa anatoka mrima, au bara basi angesemwa sana ila ni mzenji nae ��
ReplyDelete