Mwandishi Seif Hassan enzi za uhai wake
MAMIA ya wananchi, Waandishi wa habari wakiwa
wameubeba mwili wa Marehemu mwandishi wa Habari wa Radio Jamii Mkoani na
Mwanafunzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari Time School and Journalism (TSJ)Tawi
la Pemba, Seif Hassan Mohamed kuupeleka katika makazi yake ya Mwisho.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
WAUMINI mbali mbali wa Dini ya Kiislamu wakimswalia Marehemu
Seif Hassan Mohamed, aliyefariki dunia baada ya kupata ajali jana majira ya saa
moja na nusu usiku huko Mkoani(Picha na
Haji Nassor, PEMBA.)
SHEKH Salmin Sheha Ussi, akiwaongoza wananchi katika
mazishi ya Mwandishi wa habari wa Radio Jamii Mkoani Seif Hassan Mohamed,
aliyefariki dunia jana usiku na kuzikwa kijijini kwao Stahabu Mkanyageni Wilaya
ya Mkoani.(Picha na Abdi Suleiman,
PEMBA.)
WANANCHI mbali mbali Kisiwani Pemba wakifukia kwa mikono kaburi la Mwandishi wa Habari wa Radio Jamii Mkoani Sif Hassan Mohamed, aliyefariki dunia jana Usiku na kuzikwa huko kijijini kwao Stahabu Mkanyageni Wilaya ya Mkoani.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
No comments:
Post a Comment