Habari za Punde

JK alipoichagiza dunia kusaidia elimu mbele y amaelfu ya wakaazi wa Jiji la New York

  Umati wa  wakazi wa jiji na  New York waliojitokeza katika  tamasha hilo fedha zinazopatikana kupitia  tamasha hilo  hupelekwa kusaidia masuala mbalimbali ya kijamii. Tamasha hilo lilitumbuizwa na wanamziki maafuru akiwamo Rihanna ambaye ametangazwa kuwa Balozi wa  Elimu.
  Rais Mstafu Jakaya Kikwete, na Kamishna wa Kamisheni  ya Kimataifa kuhusu elimu akizungumza  mbele ya umati wa  wakazi wa jiji la  New York katika tamasha la Global Citizen Festival lililofanyika Central Park. Kupitia  tamasha hilo,  Kikwete aliichagiza jumuiya ya kimataifa kuchangia na kuwekeza katika elimu kwa  mustakabali wa kizazi  cha sasa na kijacho. Pamoja naye   ni Makamishna wenzie, Waziri Mkuu wa Norway Erna Solberg na  aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Australia  Julia Gillad.

 Rais Mstaafu akibadilishana mawili matatu na  Waziri wa  Mazingira wa Nigeria   Amina Mohammed ambaye naye alikuwa mmoja  wazungumzaji katika tamasha hilo
 Rais Mstaafu Kikwete  akisalimiana na  Balozi wa  Marekani katika Umoja wa Mataifa,  Samantha  Power  walipokutana kwenye tamasha hilo.



Na   Mwandishi  Maalum,New  York

Rais  Mstaafu  wa Tanzania,  Jakaya Mrisho Kikwete, amasema, Afrika  itandelea kubaki  nyuma kielimu ikiwa     jitihada za makusudi  hazitafanyika kuwekeza katika elimu. 

Ametoa kauli hiyo jana jumamosi mbele ya maelfu kwa mamia ya wakazi wa  Jijini la New York waliofurika  Central Park kuhudhuria  tamasha  maarufu  lijulikanalo kama  Global  Citizen Festival.

Tamasha hilo ambalo  hufanyika kila mwaka    huwaleta pamoja   viongozi  kwa  kada mbalimbali,  wanaharakati na  idadi kubwa  ya  waungaji mkono     wa  juhudi za kuutokomeza umaskini uliokidhiri na      limeandalia na  mtandao  wa Uraia wa Kimataifa ( Global Citizen) kwa  pamoja  na   Ushirikiano wa  Kimataifa kuhusu Elimu ( Global Partnership for Education) .

Aidha  fedha zinazopatika kupitia  tamasha hilo  hutumika katika kusaidia masuala  ya kimandeleo kama yakiwamo  ya afya, elimu,  mazingira,   usalama wa chakula  pamoja na masuala yanayohusu  wanawake na watoto  wa kike.

Ni  katika  tamasha hilo ambalo  mwaka  huu limelenga  pamoja na    masuala mengine, fursa ya elimu kwa watoto  wote  ambapo,    Rais  Mstaafu Kikwete ambaye pia ni Kamishna katika Kamisheni  ya Kimataifa kuhusu Elimu,   ameitaka  jumuiya ya kimataifa  kupitia hadhara hiyo kusaidia  na kuwekeza katika eneo hilo muhimu  kwa mustakabali wa kizazi cha sasa na  kijacho.

“ Afrika  yangu, itakuwa makazi ya vijana bilioni moja ifikapo mwaka 2050, na tayari  ipo nyuma kielimu” akasema Kikwete na kuongeza. “Kama  hatutawawezesha  vijana wote sasa kwa kuwapatia ujuzi na maarifa , uchumi  utapoteza kiasi  cha dola 1.8 trilioni na watoto    800 milioni  hawata kuwa shuleni ifikapo mwaka 2030. Na hii ni gharama  ya kutoelimisha  sasa”

Rais Mstaafu aliyezungumza na halaiki hiyo  kwa pamoja na Makamishna wenzie, Waziri Mkuu wa  Norway Bi. Erna Solberg  na  Waziri  Mkuu wa zamani wa Australia, Bi. Julia Gillard ambaye ni  pia ni Mwenyekiti wa  Ushirikiano wa Kimataifaka kuhusu Elimu ( GPE).Amesisitiza kwamba  “  Ni lazima tujenge kizazi kinachojifunza kwa kuogeza  fedha kiasi cha dola  3 trilioni ifikapo  mwaka 2030. Washirika  wa maendeleo ni  lazima waungane nasi katika misheni yetu hii, na sehemu kubwa  ya fedha lazima zitoke  katika vyanzo  vya mapato vya ndani”.

Katika harakati hizo za kuwafikishia  fursa ya elimu  watoto wote wa  kike na  kiume,  Global  Partnership for Education  and  Global Citizen,  wamemtangaza mwanamziki  maarufu wa Marekani Rihanna kuwa  Balozi wa  Elimu ambapo   kupitia   Taasisi yake ya  Clara Lionel watafanya kampeni ya  pamoja na   Global Partinship  for education  na  Global Citizen  kuhakikisha  kwamba watoto wote wa kike na wa kiume wanapa fursa ya elimu bora.

Jukumu jingine la mwanamziki huyo ni pamoja na kuwahamasisha   viongozi wa dunia kuunga mkono  uwekezaji   katika elimu nchini mwao.

Rihanna  na wanamuziki wengine maarufu alitumbuiza katika tamasha hilo. 


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.