Habari za Punde

Taarifa kwa Umma Muonekano wa Tovuti ya ZSSF..

MUONEKANO MPYA WA TOVUTI YA ZSSF.

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) ambao ni mfuko 

pekee wa hifadhi ya jamii Zanzibar,  unapenda kuwataarifu 

wanachama wake na jamii kwa ujumla kwamba, kutokana na 

mabadiliko ya kiteknolojia na mahitaji ya wanachama wake 

imeboresha huduma zake kwa sasa kupitia Tovuti yake.

 Tovuti hiyo ya ZSSF, www.zssf.org  ilikuwa ikifanyiwa marekebisho makubwa miezi michache iliyopita ili kuweza kukidhi mahitaji ya  wanachama wake na kuondosha kasoro zilizopo.  Kwa sasa kupitia Tovuti ya ZSSF ambayo pia imeunganishwa  na mitandao mengine ya kijamii ikiwemo face book, inawawezesha wanachama wake kufanya usajili, kuona michango yao na kuuliza maswali  popote walipo. Pia wanaweza kutoa malalamiko au mapendekezo yeyote kuhusiana na ZSSF.

Kutokana na maboresho hayo, wanachama  wanaweza  kujua zaidi 

kuhusiana na Mfuko  unaojumuisha Mfuko Mkuu ambao ni lazima 

kwa kila muajiriwa kujiunga na Upo Mfuko wa Hiari (ZVSSS) 

kwa  Wajasiriamali na Mtu  yeyote anaweza kujiunga nao.

Aidha tovuti hiyo inatoa taarifa za Miradi na Uwekezaji wa Mfuko 

kama vile Maduka ya Mwanakwerekwe , Mnara wa Kumbukumbu 

ya miaka 50 ya mapinduzi  ya Zanzibar, Viwanja vya Kariakoo , 

Tibirinzi pamoja na  habari na matukio ya Mfuko kwa jamii.

Mfuko wa Hifadhi ya jamii  Zanzibar  unapenda kuwahakikishia wanachama wake na jamii kwa ujumla kwamba ,Tovuti yake itaendelea kuwa na muonekano mpya kadri siku zinavyoendelea kupitia huduma zake. Pia inawaomba wanachama na wasiokuwa wanachama kutembelea Tovuti hiyo ili kuhabarika na kuuliza masuali na kutoa maoni yao kwa lengo la kuimarisha Mfuko wa ZSSF.
Imetolewa na :

Kitengo cha Masoko na Uhusiano.

MFUKO WA HIFADHI YA JAMII ZANZIBAR

MAKAO MAKUU KILIMANI MNARA WA MBAO. S.L.P 2716

SIMU:+255-24 2230242,   FAKSI:+255242232820,

Barua pepe:info@zssf.,   Tovuti.www.zssf.org.

“ZSSF NI UFUNGUO WA MAISHA YA BAADAE”
 ###

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.