STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Pemba 9.11.2016
![---](file:///C:\Users\user\AppData\Local\Temp\msohtmlclip1\01\clip_image004.gif)
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein ameeleza
kuwa ili nchi ipige hatua katika kuimarisha maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na
kijamii ni lazima suala la umoja na mshikamano lipewe kipaumbele.
Mama Mwanamwema Shein aliyasema hayo huko
katika ukumbi wa Ikulu ndogo Chake Chake Pemba, wakati alipokuwa na mazungumzo
na Wajumbe wa Umoja wa Wake wa Viongozi wa Majimbo kutoka Pemba.
Katika maelezo yake, Mama Shein ambaye
ndio mlezi wa Umoja huo, alisema kuwa kuna kila sababu kuzidisha ushirikiano
miongoni mwa wajumbe wa Umoja huo ili uweze kufikia lengo lililokusudiwa ikiwa
ni pamoja na kuendelea kuisaidia jamii.
Mama Shein, aliwasisitiza wake hao wa
viongozi pamoja na wajumbe wote wa Umoja huo, kuwa ni lazima juhudi za makusudi
za kimaendeleo zikachukuliwa katika kipindi hichi ili kuviachia vizazi vijavyo
uchumi na maendeleo endelevu.
Nae Mama Asha Balozi, Mke wa Makamo wa
Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaeleza Wajumbe hao umuhimu wa Umoja huo sambamba
na malengo na madhumuni yake katika kuisaidia jamii, kukiimarisha Chama Cha
Mapinduzi pamoja na kuileta nchi maendeleo.
Mapema Mama Fatma Karume alieleza haja
kwa mashirikiano na maelewano mema kwa wake wa viongozi kwa kutambua kuwa na
wao ni sehemu ya viongozi hivyo, hawana budi kushirikiana na jamii jambo ambalo sio geni katika kwa Zanzibar
tokea wakati wa kudai uhuru wake.
Nao Wajumbe hao wa Umoja huo kutoka Pemba
waliahidi kuendeleza mashirikiano katika kuhakikisha Zanzibar inapata maendeleo
na Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kushika hatamu.
Wajumbe hao walimuhakikishia Mama Shein
kuwa wataendelea kumuunga mkono na kushirikiana nae kwa nguvu zao zote ili
kuhakikisha umoja huo unaimarika.
Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee,
Vijana, Wanawake na Watoto Maudline Castico aliwaeleza wanajumuiya hao
kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
chini ya uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Kohamed Shein itaendelea kuwaunga mkono na kuwasaidia, wazee, vijana,
wanawake na watoto katika kutatua changamoto zinazowakabili.
Pamoja na mambo mengineyo Umoja huo wa
Wake wa Viongozi ambao pia, huwashirikisha Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa
Kuteuliwa na wale wa Viti Maalum, uliwachagua viongozi mbali mbali kwa upnde wa
Pemba akiwemo Zulfa Mmaka kuwa Naibu Katibu wa Umoja huo, Msaidizi Mshika fedha
Tatu Mohammed na Makamo Mwenyekiti Zume Ali Othman.
Mama Shein amerejea leo Unguja kutoka kisiwani
Pemba ambapo akiwa kisiwani humo alikutana na Wawakilishi wa Majimbo ya Pemba,
viongozi na wajumbe wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) wa Mikoa yote ya
Pemba, alikutana na viongozi wa madhehebu ya dini ya Kikristo pamoja na kuchangia
ujenzi wa Madrasatul Nuur Juhud iliyopo Micheweni na hatimae kukutana na wake
wa Wawakilishi wa Majimbo ya Pemba hapo jana.
Rajab Mkasaba,
Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment