Na Haji Nassor, Pemba
WAZAZI wenye watoto wanaoishi kwenye
nyumba za maendeleo kisiwani Pemba, wametakiwa kuwaangalifu na kuwapiga
marufuku watoto wao kuacha mtindo wa kupururuka kwa kutumia makalio,
wanaposhuka ngazi za nyumba hizo.
Watoto
hao wamebainika kupururuka kuanzia hata ngazi ya nne wanaposhuka chini na
wakati mwengine wakiwa zaidi ya watatu jambo ambalo linaweza kusababisha maafa
pindi wakianguka.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti majirani wa nyumba hizo, wamesema
imekuwa ni mtindo kwa watoto wanaoishi nyumba hizo kujihatarishia maisha yao.
Amina
Khamis Makame wa Mtemani Wete, alisema mtendo huo zaidi hufanywa kati za usiku
au kwa siku za mapunziko wanapokua hawakwenda chuoni au skuli.
“Hupururuka
kwa kutumia makalio yao kutoka ngazi ya nne hadi ya chini, na wakati mwengine
huwa zaidi ya watatu, ni hatari maana akikosa mtelezo anaweza
kuanguka’’,alifafanua.
Nae
Mwanahija Kombo Omari wa eneo hilo, alisema lazima wazazi wa watoto hao,
wajiwekee mikakati ya kuwazuia watoto hao kabla halijatokeza kubwa.
Kwa
upande wake Said Khamis Juma wa Madungu Chakechake, alilizishauri kamati za
sheha kuwaita wakaazi wa nyumba hizo ili kuwapa habari za watoto wao.
Mwadini
Ali Mchama ‘bamcha’ alisema imekuwa ni kwaida hata kwa watoto wasioishi nyumba
hizo za maendeleo kufanya mchezo wa kuteleza kwenye mgomgo wa ngazi
hizo.
Mmoja
wa wazazi wanaoishi kwenye nyumba hizo za maendelo za Madungu aliejitambulisha
kwa jina moja la Salum, alisema imekuwa vigumu kuwazuia watoto wa familia nyengine.
“Mwandishi
miaka hii kila mmoja analea mwanawe, wangu hawaingia kwenye mchezo, huu lakini
wa wenzangu wasiokatazika wanaendelea’’,alifafanua.
Nae
mzazi Hassina Mjaka Mathias wa Mtemani Wete, alisema ghorofa analoishi yeye kwa
mwaka mmoja sasa wamefanikiwa kuwazuia watoto na hasa baada ya kutokezea mmoja
wao kuanguka.
“Alikuja
mtoto kwangu kuja kutembea, wakati anafanya mtelezo huo aliangua ngazi wa chini
na kuumia ndio maana wazazi tulikutana na kupiga marufuku’’,alifafanua.
Mtoto
Himid Salum anasema kwa sasa mchezo huo wameuawacha, ingawa wanaofanya ni
wenzao wasioishi kwenye nyumba hizo.
“Wanaofanya
ni watoto wale wanaokuja mara moja kwa kutumwa kwenye nyumba hizi za ghorofa,
lakini sisi tumeshaacha mchezo huo wa kutekeleza’’,alifafanua.
Sheha
wa shehia ya Mtemani, Mrisho Juma Mtwana alisema alishapiga marufuku kwa muda
mrefu juu ya mchezo huo kwa kushirkiana na wazazi husika.
“Nashukuru
tumefanikiwa kuuzima mchezo wa kuteleza, ambao ulishashashiika kasi, lakini
sasa twashukuru baada ya kukutana na wazazi hakuna tena michezo
hiyo’’.alifafanua.
Katika
miaka ya hivi karibuni watoto wanaoishi na wasioishi kwenye nyumba za maendeleo
wamekuwa wakiendesha mchezo wa kuteleza kwa kutumia kuza za vidaraja vilivyomo
kwenye nyumba hizo.
No comments:
Post a Comment