Habari za Punde

Kaimu Katibu UVCCM afungua mafunzo ya Ujasirimali kwa Makatibu na Wenyeviti wa UWT kata18 Mkoani Kaskazini Unguja

 Mwenyekiti wa UWT wa Uwt Mkoa wa Kaskazini akimkaribisha Mgeni Rasmi katika Ufunguaji  wa Semina ya Mafunzo ya Ujasiliamali Shaka Hamdu Shaka Kaimu Katibu Uvccm Taifa
Kaimu Katibu UVCCM  Taifa Shaka Hamdu Shaka akizungumza katika kufungua Semina hiyo ya mafunzo ya Ujasilia mali kwa Makatibu na Wenyeviti wa UWT kata18 Mkoani Kaskazini Unguja Alisema''Lazima tuhamasishane dhana hii ya Tanzania ya viwanda haihitaji mamilioni ya pesa tunaweza kuanzisha viwanda vidogo  vidogo  na vijana wakapata ajira, kukamilika kwa mafunzo haya  na tija yake ikaonekana ndani ya jamii naamini tutakuwa tumepunguza malalamiko ya vijana na wakinamama,  jukumu kubwa sasa ni kuwasimamia, kuwaendeleza  ili mkikamilisha mafunzo haya  malengo yaweze kufikiwa , na pia tunataka  mkawe kielezo kizuri  cha uhalisi wa jambo hili katika maeneo yenu, hata hizi million moja  nilizowachangia naelekeza zikanunuliwe malighafi ili kuongeza  uzalishaji na kuimarisha mfuko wenu muda huu mkiendelea na mafunzo"
Mbunge wa viti  Maalum na mfadhili Mkuu wa mafunzo hayo Mhe  Malembeka akimkabidhi moja ya Bidhaa  iliyo tengenezwa  katika Mafunzo hayo aina ya batiki kaimu katibu mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka katika ufunguaji wa semina ya mafunzo ya  Ujasiria mali kwa makatibu na wenyeviti UWT kata 18 Mkoani Kaskazini Unguja.
Baadhi ya Washiriki wa Semina hiyo
Kaimu Katibu  Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka wa pili kulia akionyeshwa aina mbali mbali za Batiki zilizo tengenezwa na Washiriki wa Semina ya mafunzo ya ujasiliamali kwa maklatibu na wenyeviti UWT Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Mbunge wa viti  Maalum na mfadhili Mkuu wa mafunzo hayo Mhe  Malembeka wa kwanza kushoto akimuonesha na kumfafanulia Ndg:Kaimu Katibu Mkuu namna kemikali zinazo baki mara baada ya utengenezaji wa batiki

(picha zote na Fahadi Siraji)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.