STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 6.2.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amewaapisha
viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viongozi walioapishwa
ni Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Jaji Rabia Hussein
Mohamed kuwa Mwenyekiti wa Mahkama ya Rufaa ya Idara Maalum za SMZ, Asha Ali
Abdalla ambaye anakuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ambaye kabla ya uteuzi huo
alikuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala
Bora.
Wengine ni Yakout Hassan Yakout ambaye anakuwa Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Seif
Shaaban Mwinyi ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais, Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora anayeshughulikia Utumishi wa Umma.
Hafla hiyo, ilifanyika
Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa
Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Kadhi Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Khamis Haji.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed
Mahmoud, Wakuu wa Vikosi vya SMZ, Meya
wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Washauri wa Rais wa
Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment