STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 6.2.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein ametoa pongezi kwa viongozi wote waliopandishwa vyeo na
kuapishwa katika hafla iliyofanyika leo Ikulu jijini Dar-es-Salaam na kueleza
kuwa Jeshi la Ulinzi la Tanzania limejijengea sifa kubwa ndani na nje ya
Tanzania.
Dk. Shein alisema hayo
katika hafla ya kumuapisha Mkuu mpya
wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, na viongozi wengine akiwemo Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ,
Mabalozi na wengineo.
Katika hotuba yake
fupi ya kusalimia na kutoa pongezi kwa viongozi hao walioapishwa, Dk. Shein
alisema kuwa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania limeweza kufanya kazi kubwa ya ulinzi
hapa nchini sambamba na kuwa na nidhamu ya hali ya juu ambayo imeipa sifa kubwa
Tanzania.
Pamoja na hayo, Dk.
Shein alimpongeza Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Davis Mwamunyange kwa
ufanyaji kazi wake katika muda wake wote wa kazi na kumpongeza na kumuahidi Mkuu
huyo mpya wa Jeshi la Ulinzi Jenerali Mabeyo kuwa Serikali ya Mapinduzi ya itaendelea
kutoa ushirikiano mkubwa kwake na kwa Jeshi hilo.
Sambamba na hayo, Dk.
Shein alitumia fursa hiyo kumpongezi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
John Pombe Magufuli kwa kumualika katika hafla hiyo kubwa.
Mabeyo aliteuliwa
Februari 2 mwaka huu na Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania John Magufuli kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Jenerali Davis
Mwamunyange.
Wakati huo huo, Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amewaapisha
viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbali mbali katika Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viongozi walioapishwa
na Rais Dk. Shein ni Ibrahim Mzee Ibrahim ambaye anaendelea kuwa Mkurugenzi wa
Mshatka (DPP), Jaji Rabia Hussein Mohamed kuwa Mwenyekiti wa Mahkama ya Rufaa
ya Idara Maalum za SMZ, Asha Ali Abdalla ambaye anakuwa Katibu Mkuu wa Wizara
ya Afya ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Wengine ni Yakut Hassan Yakout ambaye anakuwa Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Seif
Shaaban Mwinyi ambaye anakuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais, Katiba,
Sheria, Utum,ishi wa Umma na Utawala Bora anayeshughulikia Utumishi wa Umma.
Hafla hiyo ilifanyika
Ikulu mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa
Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa
Zanzibar Said Hassan Said, Mawaziri, Manaibu Mawaziri, Kadhi Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Khamis Haji.
Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed
Mahmoud, Wakuu wa Vikosi vya SMZ, Meya
wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Washauri wa Rais wa
Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment