Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Dk.SHEIN Awaapisha Watendaji Ikulu leo.

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)  Bw.Ibrahim Mzee Ibrahim wakipitia hati za kiapo na Jaji Rabia Hussein Mohamed kuwa Mwenyekiti wa Mahkama ya Rufaa ya Idara Maalum za SMZ,kabla ya kuapishwa kushika nafasi walizoteuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) leo hatika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Unguja. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw.Ibrahim Mzee Ibrahim kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Jaji Rabia Hussein Mohamed kuwa Mwenyekiti wa Mahkama ya Rufaa ya Idara Maalum za SMZ,hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bi Asha Ali Abdulla  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,kabla alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora,hafla iliyofanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw.Seif Shaaban Mwinyi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais,Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora anayeshuhulikia Utumishi wa Umma,katika hafla iliyofanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo

Baadhi ya Mawaziri wa Wizara mbali] mbali  waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa watendaji katika Wizara za Serikali ya Mapinduzi leo ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 06/02/2017.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.