Na.Haji Nassor - Pemba.
WIZARA ya Kilimo, Maliasili, Mifugo
na Uvuvi kisiwani Pemba, imesema ikiwa hadi Oktoba 23 mwaka huu, wananchi
wanaodaiwa zaidi ya shilingi bilioni 1. 492 zinazotokana na ukodishwaji wa
mikarafuu hawajalipa fedha hizo, Wizara hiyo itawakabidhi kwa ZAECA.
Kauli hiyo,
imetolewa na Afisa Mdhamini wa wizara hiyo, kisiwani humo Sihaba Haji Vuai,
wakati alipokuwa akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, juu ya mwenendo wa
ukodishaji na namna ya wananchi waliokodi walivyolipa fedha hizo.
Alisema
tayari mashamba 1,451 yameshakodishwa kwa wananchi mbali mbali kisiwani Pemba,
ambapo kama ingekuwa wameshalipa, serikali ingepata zaidi ya shilingi bilioni
2.393, ingawa hadi sasa, ni zaidi ya shilingi milioni 900.661 zilizokwishalipwa
.
Alisema
ambacho bado kimo mikononi mwa wananchi hao waliokodia amshamba ya mikarafuu ya
serikali, ni shilingi bilioni 1.492 ambazo hizo, zinatakiwa kulipwa sio zaidi
ya Oktoba 23, mwaka huu.
Alisema
kuanzia Oktoba 24, mwaka huu wadaiwa hao kama hawajalipa fedha hizo, wizara
hiyo itawakabidhi kwa Mamlaka ya Kuzuia rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar
ZAECA, ili kuwashikilia kisheria.
“Zoezi la
ukodishaji bado linaendelea, lakini kwa sasa fedha nyingi bado ziko mikononi
mwa wananchi, waliokodi mashamba kwa hiari zao na mikataiba iliwataka walipe
ndani ya wiki mbili, lakini kuanzia Oktoba 24, basi tutawakabidhi kwa wenzetu
ZAECA”,alifafanua.
Akatika
hatua nyengine Afisa Mdhamini huyo, aliwataka wananchi wema wanaopenda
maendeleo ya nchi hii, kuendelea kuyafichua mashamba ya serikali na kuyaripoti
kwa mamla husika, ili yarudi serikali kisheria.
Alieleza
kuwa, katika zoezi hilo lililoanza Julai 1, mwaka huu lilisaidia kuyaibua
mashamba kadhaa mapya, ambayoa kwa muda mrefu serikali ilikuwa haijawayatambua.
Alisema kwa
mfano kwenye wilaya ya Micheweni walitarajia kuwa na mashamba …lakini baada ya
wananchi wema kuona umuhimu wa kuyafichua mashamba hayo, kwa msimu huu
wameyapata mashamba …..
“Aidha kwa
mfano kwenye wilaya ya Chakechake shehia za Gombani, Kwale, Tibirinzi na
Mkoroshoni tulikuwa hatuna mpango wala uwelewa kuwa kuna mashamba ya mikarafuu
lakini kwa sasa tunayo mashamba 10 mapya”,alisema.
Aidha
alifafanua kuwa kwenye wilaya ya Micheweni, walijiwekea malengo ya kuwa na
mashamba 50 pekee, ingawa wakati zoezi hilo likiendelea limeibua mashamba 169,
sawa na ongezeko la mashamba 119 yaliokuwa yakimilikiwa na wananchi kinyume na
sheria.
Hata hivyo
alisema sio kweli kuwa zoezi hiloi lengo lake ni kuwany’ang’a wananchi mashamba
yao, bali lengo ni kutaka mali ya serikali kurudi mikononi mwake na wananchi
walipokwisha tumia panatosha.
Alisema
wakati zoezi hilo likitaka kuanza mapema mwaka huu, walidhamiria kuwa
watayaibua mashamba ya ya serikali 1,525 ingawa hadi sasa wakati zoezi halijamalizika
tayari wameshayapaa mashamba ya eka tatu tatu 1,451 pamoja yake matano makuwa
likiwemo la Makuwe, Daya Mtambwe, Kianyasini, Gando na Mkoani.
Kwa upande
wake Afisa Mashamba ya serikali kisiwani Pemba, Haji Mussa Haji, alisema kwa vile
zoezi hilo linazingatia sheria zilizopo, yapo mashamba 84 waliyoyakodisha
kinyume na taratibu, wamesharejeshewa wenyewe, baada ya kuyonyesha nyaraka
halali.
“Tunapokodisha
mmiliki wa shamba akija na nyaraka basi tunakaa nae meza moja, kuipitia kifungu
kwa kifungu na aya kwa aya, na tukibaini wakabidhiwa wenyewe, kama ambapo sasa
tumeshafanya kwa madhamba 84, yakiwa 20 Kusini na 64 kaskazini
Pemba”,alifafanua.
Aidha Afisa
huyo, alisema pia zipo shilingi milioni 528 ambazo hazijalipwa kama kifuta
jasho kwa wananchi wale ambao walikuwa wakiyalea mashamba hayo ya serikali,
ambapo hupatiwa fedha hizo, hata kama aliekodi ndie anaelilea.
Wakati huo
huo Mdhamini wa ZAECA Pemba, Suleiman Ame Juma
alisema, wako tayari kushirikiana na wizara yoyote ikiwemo hiyo ya Kilimo,
katika kutetea na kunusuru mali ya umma isiishie kwenue mikono ya wachache.
“Sisi hiyo
ni kazi yetu kwa mujibu wa sheria, tunaweza kuwahoji na kuwashikilia kisheria,
mtu yeyote ambae anaenda kinyume na uwajibikaji wa fedha za umma”,alifafanua.
Zoezi la ukodishaji wa mashamba ya serikali
ambao ulianza Julai 1, mwaka huu, umesaidia kwa kiasi kikubwa kuyafichua
mashamba kadhaa ya serikali ambayo, yalikuwa mikononi mwa wananchi wa kawada.
No comments:
Post a Comment