NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAFANYAKAZI wa sekta za umma nchini, wamependekeza
kusimamiwa kikamilifu kufanyiwa uchunguuzi wa afya zao kila baada ya muda, kama
sheria ya Afya na Usalama Kazini no 8 ya mwaka 2005, ilivyoelekeza kwenye
kifungu chake cha 58 cha sheria hiyo.
Walisema
muajiri amekuwa makini na kulazimisha kumfanyia uchuguuzi wa kiafya, mtu
anaetaka kumuajiri, ambapo hilo limetajwa kwenye sheria ya uajiri, ingawa baada
ya ajira sheria ya Afya na Usalama Kazini ya kufanyiwa tena uchunguuzi,
haitekelezwi.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, wafanyakazi hao walisema, wapo
baadhi yao wamekuwa wakimaliza muda wa utumishi, bila ya kufanyiwa uchunguuzi
wa afya zao.
Walisema
wanashangaa kuona sheria halali ipo, inayomlazimisha muajiri, kila baada ya
muda kuwafanyia uchunguuzi wa afya, ingawa hilo limebakia kwenye vitabu vya
sheria bila ya kutekelezwa.
Mmoja
kati ya aliekuwa mfanyakazi wa wizara ya Afya Pemba sehemu ya udereva Suleima
Mohamed Suleiman (74), alisema yeye tokea mwaka alioajiriwa mwaka 1977 na hadi
alipostaafu miaka 35 baadae, hakumbuki kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.
Alisema
akiwa ndani ya utumishi, alikumbana na changamoto kadhaa, ikiwemo hata kukukosa
likizo, fedha za nje ya wakati wa kazi, pamoja na kukosa kufanyiwa vipimo kila
muda.
“Kwanza
sijui kama kuna sheria inayomlazimisha muajiri kunichunguuza kiafya, naona
nafanya kazi tu, sina likizo na hata ikitokezea naenda hospitali, basi gharama
huwa zangu binafsi”,alifafanunua.
Nae
aliekuwa dereva Kamisheni ya Utalii Pemba Khamis Sultan Hemed (67), anasema
yeye alianza kazi mwaka 1971, lakini uchunguuzi wa afya, anakumbuka mwaka huo
wakati anaajiriwa.
Hata
hivyo dereva huyo aliestaafu mwaka 2000, alisema hana hakika kuwa waajiri,
sheria hiyo ya Afya na Usalama Kazini hasa kifungu cha 58 ikiwa, wanakifahamu.
“Nilitarajia
muajiri kifungu hicho akitekeleze, maana iwapo atakipuuza, atakosa mfanyakazi
imara na mwenye afya bora, kwenye kutekeleza majukumu yake”,alieleza.
Mohamed
Amran Massoud dereva Shirika la Utangaazaji Zabzibar ZBC Pemba, alisema kwenye
wizara yake, yeye ameshashiriki zaidi ya mara nne, kufanyiwa uchunguuzi wa afya
yake.
Mohamed
Juma Rashid ambae ni Afisa Utumishi wa wizara hiyo, alisema kila mwaka wizara
hiyo, imekuwa ikiwaleta madaktari, kwa ajili ya kuchunguuza afya za watendaji
wake.
“Sisi
hatukubali kuwaacha wafanayakazi bila ya kuwachunguuza afya, maana ndani yake
tunapata kujua nani anapaswa kupangiwa kazi ngumu na nani hapaswi”,alifafanua.
Afisa
Mdhamini wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati Pemba Juma Bakari Alawi,
alisema yeye tokea ashike nafasi hiyo mwaka wa pili sasa, hajawahi kuwafanyia
uchunguzi wa afya wafanyakazi wake.
“Tatizo
hasa ni ukosefu wa bajeti kwa ajili ya shughuli hiyo, lakini katika bajeti
ijayo ya mwaka 2018/2019, tutaingiza kifungu maalumu, ili kuwafanyia uchunguuzi
watendaji wetu”,alifafanua.
Afisa
Mdhamini wizara ya Afya Pemba Bakar Ali Bakar, alikiri kuwa hata ofisi yake
haijawahi kuwafanyia uchunguzi wa kiafya wafanyakazi wake, kama sheria hiyo
inavyoelekeza.
“Kwa
upande wa wizara yetu, sio tatizo la bajeti bali ni mifumo ya ndani ya wizara
tu bado haijakaa sawa, lakini sasa tumeshajipanga na tutawafanyia”,alifafanua.
Wafanyakazi
wa Wizara ya Miundombinu Pemba, Khamis Massoud na Asha Mohamed, walisema wao
kila mwaka wamekuwa wakifanyiwa uchunguuzi wa afya zao, na imekuwa ikizaa
matunda.
Waziri
wa Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe:
Haroun Ali Suleiman, alisema wakati sheria ipo, hakuna namna kwa waajiri bali
ni kuhakikisha wanaitekeleza.
“Mkazo
kwa waajiri wasiuweke tu wakati wanapotaka kuajiri ndio wawafanyie vipimo, bali
hata baada ya muda kama sheria ilivyoelekeza wawafanyie uchunguuzi”,alifafanua.
Sheria
ya afya na usalama kazini no 8 ya mwaka 2005 ambayo ina vifungu 133 na
sehemu 13, kwenye kifungu chake cha 58
kimeeleza kuwa “
baada ya muda wafanyakazi watachunguuzwa afya zao na madaktari wenye sifa, ambao wataidhinishwa na Mkurugenzi”.
Aidha
kifungu hicho kimeendelea kueleza kuwa, gharama
za uchunguuzi zitalipwa na Muajiri.
No comments:
Post a Comment