Waziri wa Afya Mh Mahmoud Thabit Kombo akikagua ujenzi wa kituo cha Afya kijiji cha Ngomeni, shehia ya Mgelema Chakechake, Pemba
NA HAJI NASSOR, PEMBA
WIZARA ya Afya Zanzibar, imewaeleza wananchi wa Ngomeni
shehia ya Mgelema wilaya ya Chakechake Pemba, kuwa ujenzi wa kituo chao kipya
cha afya unatarajiwa kukamilika si zaidi ya miezi mitatu ijayo, kama mambo
walioyapanga yatakwenda vyema.
Kauli
hiyo imetolewa na waziri wa Wizara hiyo Mhe: Mahamoud Thabiti Kombo hivi
karibuni, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kijijini hapo, ikiwa ni
sehemu ya ziara yake alioifanya ghafla kuangalia ujenzi maendeleo ya ujenzi wa
jengo hilo.
Alisema
baada ya ujenzi huo sasa kukabidhi wajenzi wa wizara yake, na kama vifaa
walivyovipanga watavipata kupitia bajeti yao kuu, miezi mitatu ijayo, wananchi
wa kijiji cha Ngomeni, wataanza kupata huduma za kiafya kama walivyowananchi
wengine.
Waziri
huyo alisema mikakati ya serikali kupitia Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015 hadi
2020 ni kuona wananchi wote wanapata huduma za kitabibu bila ya ubaguzi wa
chama wala rangi ya watu.
Alisema
ndio maana baada ya Rais wa Zanzibar kutembelea kijiji hicho na kutoa agizo la
ujenzi wa kituo cha afya kijijini hapo, wizara yake ilijipanga haraka
kutekeleza agizo hilo.
“Sisi
kama wizara, kazi yetu ni kuwafikishia wananchi huduma za kiafya popote pale
walipo, ingawa baada ya kiongozi wetu mpendwa kutoa agizo lake, na sisi
twalitekeleza”,alifafanua.
Katika
hatua nyengine Waziri huyo wa Afya, alisema baada ya ujenzi huyo kukamilika,
wananchi wasiwe na wasiwasi wa upatikanaji wa dawa na madaktari husika.
Alisema
tayari wameshapewa kibali cha kuajiria kati ya madaktari 300 hadi 350, ambapo
mongoni mwao watatoa huduma kwa kituo hicho cha cha kijiji cha Ngomeni.
“Hivi
karibuni tulishazungumza na mamlaka husika juu ya ajira za madaktari, hivyo
kibali kimeshatoka na naamini tukiajiri basi na wananchi wa Ngomeni kupitia
kituo chao cha Afya watafika”,alifafanua.’
Kuhusu
nyumba ya dakatari kwa ajili ya Kituo hicho cha Afya, alisema baadae wizara
itajenga nyumba ambayo itakuwa na uwezo wa kukaliwa na madaktari watatu kwa
wakati mmoja.
Kwa
upande wake fundi mkuu wa ujenzi wa Kituo hicho cha Afya Omar Maktuba, alisema
kikosi kazi alichonacho cha mafundi 10 na vibarua 20, kama akipewa vifaa kwa
wakati, hatarajii miezi mitatu ijayo bila ya kukabidhi jengo hilo.
“Ujenzi
kwa sasa unaendelea vyema, maana msingi wa mwanzo “foundation” iliojengwa na
mkandarasi tuliuvunja na sisi tumeshanza kwa kasi tokea August 17 mwaka huu, na
kwa kikosi nilichonacho kazi hii itamalizika kwa muda mfupi ujao”,alisema.
Katika
hatua nyengine fundi huyo Mkuu, aliwataka wananchi wa kijiji cha Ngomeni shehia
hiyo ya Mgelema, kuwapa kila aina ya ushirikiano ili ujenzi huo ukamilike kwa
wakati.
Wazo
la kujenga kituo cha afya kijijini hapo, liliasisiwa na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe: dk Ali Mohamed Shein, alipokitembelea
kijiji hicho mwishoni mwaka jana.
No comments:
Post a Comment