Tawi jipya la CCM Pandani wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba, ambalo August 8, mwaka huu, liliwekewa jiwe la msingi na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Mhe; dk Ali Mohamed Shein, ambapo kwa sasa shilingi milioni 26, zinahitajika huku, Makamu Mwneyekiti huyo wa CCM Zanzbar, akiahidi shilingi milioni 10, mara tu CCM mkoa wa kaskazini Pemba, itakapokusanya shilingi milioni 16, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
Na.Haji Nassor - Pemba.
Na.Haji Nassor - Pemba.
CHAMA cha Mapinduzi CCM Mkoa wa
kaskazini Pemba, kimesema kinaendelea kujipanga, ili kuhakikisha wanazipata
shilingi milioni 16, kati ya shilingi milioni 26, zinazohitajika, kwa ajili ya
kumaliza hatua ya ujenzi wa tawi jipya la kisasa la CCM Pandani.
August 8, mwaka huu Makamu Mwenyekiti wa CCM
Zanzibar Mhe: dk, Ali Mohamed Shein wakati ya ziara yake ya siku nne kisiwani
Pemba, alifika kwenye tawi hilo, kwa uwekaji wa jiwe la msingi, ambapo wanaccm
wa tawi hilo, waliomba shilingi milioni 26, kwa ajili ya kumalizia ujenzi tawi hilo.
Hivyo,
aliuagiza uongozi wa CCM Mkoa wa kaskazini Pemba, kuzisaka kwa udi na uvumba
shilingi milioni 16, ambapo nae baada ya wao kuzipata fedha hizo, aarifiwe ili
akamilisheni ahadi yake ya shilingi milioni 10.
Mwenyekiti
wa CCM Mkoani humo, Mberwa Hamad Mberwa, akizungumza na mwandishi wa habari
hizi kwa njia ya simu, alisema walikuwa wanasubiri kwanza wamalize chaguzi zao
za ndani, pamoja na kumalizika kwa kikao cha baraza la wawakilishi, ili
wakutane na mwakilishi wa jimbo la Pandani.
Alisema
kikao hicho, kitakachojumuisha viongozi kadhaa wa CCM, ndio kitakachozaa wazo
na njia za kuzipata shilingi milioni 16, ambapo hapo baadae, ndio watawasiliana
na Makamu Mwenyekiti CCM Zanzibar, kwa ajili na yeye kukamilisha ahadi yake ya
shilingi milioni 10.
“Lile agizo
la Makamu Mwenyekiti wetu wa CCM Zanzibar, bado hatujalikalia kitako, lakini
muda sio mrefu tutakutana, ili kuhakikisha tunagawana majukumu, kwa lengo la kujipatia
fedha hizo”,alifafanua.
Aliongeza
kuwa, mtazamo wake anatarajia kuwashawishi viongozi hao kwamba, sio lazima
fedha taslimu ndio zinazohitajika, bali hata vifaa vya ujenzi, ili kufanikisha
ujenzi huo.
Alisema,
wanatarajia kuwafikishia machango huo viongozi kadhaa, wakiwemo wanachama wa
CCM wenyewe, viongozi wa majimbo, wilaya, Mkoa na hata maofisa wadhamani ambao
walishaonyesha nia hiyo.
“Siku ile ya
August 8, maofisa wadhamini wa kisiwani Pemba, waliomba na wao wakaingizwe
kwenye machango huu wa kumalizia ujenzi
wa tawi la CCM Pandani, hivyo siku ikifika na wao watajumuishwa”,alifafanua.
Katika hatua
nyengine, Mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa kaskazini Pemba, alisema wanaendelea
kuyajenga matawi mengine ya CCM ya Njuguni, Wete mjini, kisiwani kwa binti
Abeid na mengine ili yawe na hadhi ya
kitaifa.
Wakati
alipotembelea tawi hilo la CCM Pandani, kwa uwekaji wa jiwe la msingi, Makamu
Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe: Dk, Ali Mohamed Shein, alipongeza hatua ya wanaccm hao kuanzisha
ujenzi huo.
Alisema,
wakati umefika sasa kwa CCM, kuwa na matawi na ofisi za kileo, ambazo
zitajengwa kwa nguvu za wanaccm wenyewe, kama walivyofanya kwa wana wa ASP,
wakati wao kwa kujenga matawi na ofisi walizozirithi.
Aidha Makamu
huyo Mwneyekiti wa CCM Zanzibar, baada ya kuelezwa kuwa, zinahitajika shilingi
million 26, ili kukamilishia ujenzi huo, aliahidi kutoa shilingi milioni 10, na
shilingi milioni 16 zilizobaki, aliuagiza uongozi wa CCM Mkoa wa kaskazini
Pemba, kuzitafuta.
No comments:
Post a Comment