Habari za Punde

Mchezo wa Ligi Daraja la Pili Wilaya ya Kaskazini A Unguja Kati ya Amber na Kijni Stars Mchezo Uliofanyika Uwanja wa Mkwajuni. Timu ya Amber Imeshinda Mchezo huo Bao 6 - 0.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Pannyroyal Zanzibar Amber Resort Saleh Mohammed Said akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ufadhili wa kampuni yao kwa shughuli za Kijamii katika Kijiji cha Matemwe Mkoa wa Kusini Unguja, wakati wa mchezo wa ligi daraja la pili wilaya ya kaskazini unguja Mradi wa Zanzibar Amber Resort, inafadhili timu za Kijiji cha Matemwe.
MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Vuai Mwinyi akiikagua timu ya Amber Sports Club inayofadhiliwa na kampuni ya Pennyroyal katika mchezo wa ligi ya soka daraja la tatu Wilaya ya Kaskazini ‘A’ kati ya timu hiyo na Kijini Stars zote za Matemwe, katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa New Stars Mkwajuni
MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Vuai Mwinyi akiikagua timu ya Kijini Stars katika mchezo wa ligi ya soka daraja la tatu Wilaya ya Kaskazini ‘A’ kati ya timu hiyo na Amber Sports Club zote za Matemwe, katika mchezo huo uliochezwa  uwanja wa New Stars Mkwajuni
WACHEZAJI wa Timu ya Amber Sports Club inafadhiliwa na Kampuni ya Pennyroyal wakisaliana na timu ya Kijini zote za Matemwe wakati wa pambano lao la soka ligi daraja la tatu wilaya ya Kaskazini ‘A’,


MCHEZAJI wa Timu ya Amber Sports Club , Mwadini Ame akitafuta mbinu za kumtoka mlinzi wa timu ya Kijini Stars, Bakar Kassim, zote za matemwe wakati wa pambano lao la ligi ya soka wilaya ya Kaskazini ‘A’, katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa New Stars Mkwajuni, amber ilishinda mabao 6-0.
MSHAMBULIAJI wa Timu ya Amber , Hussein Issa Muumin akipiga ngema baada ya kushinda bao la kwanza katika mchezo wa soka ligi daraja la tatu wilaya ya Kaskazini ‘A’ kati  ya timu hiyo na Kijini Stars zote za Matemwe, katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa New Stars Mkwajuni, amber inayofadhiliwa na Kampuni ya Pennyroyal ilishinda mabao 6-0 .
Baadhi wa Mchezo wa mpira katika Kijiji cha Mkwajuni Wilaya ya Kaskazini A Unguja wakifuatilia mchezo Ligi Daraja la Pili uliozikutanisha Timu za Amber na Kijini Stars zote kutoka katika kijiji cha matemwe. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.