Habari za Punde

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Tanzania Mhe. Hamad Masauni Ziarani Wilaya ya Bunda Kukagua na Kushughulikia Changamoto za Askari Polisi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani  ya  Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akikagua moja ya makazi ya askari polisi  katika  kijiji cha Makongoro B,  kilichopo wilayani Bunda wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua na kushughulikia changamoto za makazi ya askari polisi  ambapo jumla ya nyumba mia nne  za askari polisi zinatarajiwa kujengwa nchi nzima
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani  ya  Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akisoma maelezo ya mmoja ya mtuhumiwa  aliyemkuta katika chumba cha mahabusu katika Kituo cha Polisi Bunda wakati wa ziara ya kikazi ya kupitia shughuli za utekelezaji wa mashtaka ya mahabusu walioko katika vituo vya polisi nchini.Wapili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili na wengine ni viongozi waandamizi wa kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani  Bunda
Afisa Mnadhimu wa Polisi mkoa wa Mara, Mrakibu Mwandamizi ,Jeremiah Shila  akitoa maelezo ya mwenendo wa mashtaka ya watuhumiwa walioko katika Kituo cha Polisi Bunda kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kulia) na  Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili(watatu kulia), wakati wa ziara ya naibu waziri  kupitia shughuli za utekelezaji wa mashtaka ya mahabusu walioko katika vituo vya polisi nchini. 
Naibu Waziri wa Mambo ya  Ndani  ya  Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kushoto), akifuatilia wakati mpelelezi akifunua jalada la mmoja wa  mahabusu  aliyemkuta katika chumba cha mahabusu katika Kituo cha Polisi Bunda wakati wa ziara ya kikazi ya kupitia shughuli za utekelezaji wa mashtaka ya mahabusu walioko katika vituo vya polisi nchini.Wapili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili na wengine ni viongozi waandamizi wa kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani  Bunda.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.