Habari za Punde

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Haroub.Azungumza na Uongozi na Wafanyakazi wa CAG Zanzibar. ui


Na.Raya Hamad  OR KSUUUB
Waziri nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman amesema kuwa demokrasia na Utawala bora ni nyenzo muhimu katika ujenzi wa jamii yenye umoja  mashirikiano uwadilifu na uwajibikaji ambao hujenga heshima na nidhamu katika utekelezaji wamajukumu ya  kazi

Waziri Haroun ameyasema hayo alipokutana na watendaji wakuu na wafanyakazi wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika muendelezo wa ziara  za kutembelea taasisi zilizomo ndani ya Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Utekelezaji wa kazi za  majukumu ya Serikali  unazingatia misingi ya utawala bora kama ilivyoainishwa katika Katiba za nchi na kuimarisha  uwazi na uwajibikaji kwa wananchi  hivyo amewahimiza watendaji hao kutokubali kutumiwa vibaya au kurubuniwa kwa njia yoyote  katika kutekeleza wajibu wao

“Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali ni taasisi ambayo imepewa dhamana maalum na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar hivyo suala la kujituma na  kufuata maadili ya kazi ni lazima msije mkababashwa fanyeni kazi wala hakuna kupotea kwa fedha ndani ya  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar fuateni taratibu zote za ukaguzi kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi kama inavyoelekeza  

Aidha Waziri Haroun amewaasa vijana waliopata ajira hivi karibuni kutojiingiza katika masuala ya Siasa katika utendaji wao wa kazi na kusoma vizuri sheria ya utumishi ili kuelewa kanuni na  taratibu za utumishi  pamoja na kufuata  muongozo  na majukumu yao  kazi wanazopangiwa  jambo ambalo litaleta ufanisi wa Ofisi hio

Nae Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Bi Fatma  Mohammed  Said amesema kuwa Ofisi hio inatekeleza majukumu yake Kikatiba na kwa kuzingatia Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015 -2020  na kusisitiza kuwa Katiba ya Zanzibar  1984  kifungu 112 (3) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali   anawajibika

“kuhakikisha kwamba fedha zote zinazokusudiwa kutolewa kutoka Mfuko wa Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar matumizi yake yameidhinishwa kisheria na iwapo atatosheka kwamba masharti hayo yatatekelezwa ipasavyo basi ataidhinisha fedha hizo zitolewe ”

Aidha kifungu B  kinazungumza kuwa kuhakikisha kwamba fedha zote amabazo matumizi yake yameidhinishwa yanatokana na fedha zilizomo katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar au fedha ambazo matumizi yake yameidhinishwa na sheria iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi  na ambazo zimetumika katika shughuli iliyokusudiwa na matumizi ya fedha hizo yamefanywa kwa kufuata idhini iliyotolewa kuhusu matumizi hayo

Angalau mara moja kwa mwaka kufanya ukaguzi na kutoa taarifa  juu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  hesabu zinazosimamiwa na watumishi wote wa Serikali ya  Mapinduzi  ya Mapinduzi ya Zanzibar , Hesabu  za Mahakama zote za Zanzibar, Hesabu za Tume au vyombo vyengine vilivyoidhinishwa na Katiba hii na hesabu zinazohusika  na Baraza la Wawakilishi

Bi Fatma  amesema Ofisi inaendelea kufanya kazi za ukaguzi wa hesabu katika Wizara zote za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maidara , Taasisi, Mamlaka , Mashirika na miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na washirika wa maendeleo na kutoa ripoti za Ukaguzi wa hesabu hizo  na kuwasilishwa kwa mujibu wa Katiba .

“Ripoti hizo zimekuwa zikifanyiwa kazi  na Serikali ikiwemo Kamati ya Kudhibiti na Kuchunguza Hesabu za Serikali (PAC)”alisisitiza

Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali  pia  inaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa mujibu wa Ibara ya 143(a)Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali   inashirikiana na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kufanya ukaguzi wa pamoja katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Miradi ya Umoja wa Mataifa , Benki ya Dunia , Benki ya Maendeleo ya Afrika  nk

Kupitia mashirikiano yaliyopo ya taasisi hizo Ofisi imefanikiwa kuimarisha mashirikiano na wadau mbali mbali wa ndani na nje kupitia mafunzo , mikutano  semina , makongamano na warsha mbali mbali kitaifa na kimataifa

Akielezea baadhi  malengo iloyojipangia Ofisi hio Bi Fatma  amesema ni pamoja na kuendelea kutekeleza majukumu Kikatiba ya Ukaguzi wa Hesabu , kuendelea kuimarisha uwezo wa wafanyakazi kitaaluma  katika fani mbali mbali za Ukaguzi kama vile ukaguzi wa matokeo ya utekelezaji wa program(PBB AUDIT) ukaguzi wa mazingira , ukaguzi wa komputa , ukaguzi yakinifu na ukaguzi wa aina nyenginezo

Kutoa mafunzo ya ukaguzi wa hesabu unaozingatia viwango vilivyowekwa kitaifa na kimataifa , kutoa mafunzo ya mabadiliko ya teknologia katika mifumo ya uhasibu na ukaguzi na mafunzo ya mabadiliko ya Bajeti kwa wakaguzi kutoka katika mfumo wa vifungu (line iterm) kwenda  mfumo unaozingatia matokeo (PBB)

Katika kutekeleza majukumu  na kuimarisha Ofisi  inatumia vifaa vya kisasa pamoja na kuongezeka kwa wafanyakazi wenye taaluma ambapo wafanyakazi wapya 87 wameajiriwa na kupatiwa mafunzo ya awali yakiwemo mafunzo ya sheria na kanuni za utumishi wa Umma ,usalama wa Afya, kazini , maadili ya Utumishi wa Umma pamoja na sheria za kutunza siri  ili kuongeza ufanizi na kuifanya Ofisi hio kuwa na jumla ya wafanyakazi 215

Hata hivyo Bi Fatma amesema zipo baadhi ya changamoto ambazo zinaendelea kupatiwa ufumbuzi mara tu zinapojitokeza lakini baadhi zinahitaji rasilimali kubwa ili ziweze kutatuliwa ikiwemo mabadiliko ya Teknolojia na mifumo ya fedha, uhasibu na ukaguzi

“kwa kuwa utekelezaji wa kazi za ukaguzi unakabiliwa na mabadiliko ya mara kwa mara Ofisi inaendelea na uratibu wa kuwajengea uwezo wafanyakazi wake kwa kuwapatia mafunzo ya muda mfupi na mrefu il kuendana na teknologia habari na mawasiliano kwa lengo la kuongeza ufanisi katika kazi za ukaguzi ” alisema

Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali ni Taasisi ya Katiba inayojitegemea ambapo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali ndio kiongozi mkuu wa Ofisi anaesimamia shughuli za uongozi na uendeshaji

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.