Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Jamafest
Tanzania Bibi.Joyce Fissoo akitoa ufafanuzi wa kuwepo kwa takribani programu
kumi na moja za Kiutamaduni katika Tamasha la JAMAFEST katika kikao cha
ushirikiano wa Wizara ya Maliasili na Utalii katika kuandaa Tamasha la Urithi
Festival kilichofanyika leo Jijini Arusha.
Na Anitha Jonas – WHUSM 22/07/2019 Arusha.
Tamasha la Urithi Festival kwa mwaka huu kufanyika
pamoja na Tamasha la Utamaduni la Jumuiya ya Afrika (JAMAFEST) jijini Dar es
Salaam.
Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Arusha na Katibu
Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Prof. Adolf Mkenda alipokuwa akifanya kikao
cha pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi.Susan
Mlawi kuzungumza namna ya Wizara hizo zitakavyoweza kuungana kuandaa Tamasha la
Urithi kama ilivyokuwa imeagizwa na Waziri Mkuu.
"Kwa mwaka huu itakuwa vyema kuyaunganisha
matamasha haya mawili kwani yote yana lengo moja la kutangaza Utalii wa
Kiutamaduni, na tarehe za uendeshwaji wa matamasha hayo zipo sawa" Prof.Mkenda.
Akiendelea kuzungumza katika kikao hicho
Prof.Mkenda alisema kwa sasa sekta ya utalii inataka kuongeza wigo zaidi na
kutangaza utalii kwa Kiutamaduni ikiwemo Vyakula vya Asili,Ngoma,Mila na
Desturi za Makabila mbalimbali, lengo ikiwa ni kuonyesha ulimwengu utajiri wa
Utamaduni uliyopo Tanzania,kama nchi za wenzetu wa India na China wanavyofanya.
Halikadhalika kwa upande wa Katibu Mkuu wa Wizara
ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi.Susan Mlawi alimshukuru Katibu Mkuu
huyo kwa kuridhia matamasha hayo kuunganishwa kwani lengo ni moja la kutangaza
sekta ya Utalii wa Utamaduni wa Taifa.
Pamoja na hayo Bibi.Mlawi aliendelea kufafanua kuwa
Tamasha la JAMAFEST huandaliwa na kila baada ya miaka miwili na kwa mwaka
huu Tanzania ndiyo mwenyeji na wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
ndiyo mwenye jukumu la kuandaa tamasha hilo kwa sasa kama wizara yenye dhamana
ya Utamaduni.
"Tamasha hili la JAMAFEST ni kubwa na
tunatarajia kuwa na washiriki zaidi ya elfu moja kutoka nchi za wanachama wa Jumuiya,
katika tamasha hili kutakuwa na matukio mbalimbali ambayo yataongeza chachu kwa
Sanaa za Ufundi,Maigizo ya Jukwaani,ziara ya kutembelea vivutio vya Utalii,ambapo
kila nchi wanachama itateua mtu mmoja wa kwenda kutembelea vivutio hivyo,"
alisema Bibi.Mlawi.
Halikadhalika tamasha hilo linauwezo wa kutengeneza
jukwa zuri ambalo litatangaza filamu za kiutalii za taifa kupitia shindano la
Serengeti Film Festival ambalo nalo litafanyika wakati huo.
Naye mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Urithi
Festival Prof.Martin Mhando alisema kuunganishwa kwa matamasha haya mawili
kutusaidia zaidi kutangaza utalii wa Utamaduni na pamoja na kukuza uchumi wa
nchi kwa sekta ya utalii itapata fursa ya kunadi bidhaa za Kiutamaduni ikiwemo
vinyago na michoro mbalimbali.
Halikadhali naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi
ya Jamafest Tanzania Bibi.Joyce Fissoo alisema tamasha hilo litakuwa na mambo
mbalimbali ikiwemo maonyesho ya vyakula vya asili kutoka nchi wanachama,Sanaa
za Ufundi,Mashindano ya Michezo ya Jadi na Maonyesho ya Mavazi ya Kiutamaduni.
No comments:
Post a Comment