Habari za Punde

Ujumble wa Wafanyabiashara kutokea nchini Brazil kesho Jumatatu saa tisa kamili utatua Julius Nyerere Airport

Ubalozi wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Zanzibar unapenda kuwatarifu wote kuwa ujumbe wa Tanzania uliojumuisha wafanyabiashara 12 kutoka sekta binafsi na baadhi ya wakuu wa mashirika ya umma waliokwenda kwenye ziara ya kibiashara nchini Brazil kwa siku kumi unatarajiwa kurudi nchini Tanzania kesho Jumatatu saa tisa kamili mchana kupitia uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Airport na ndege ya South African Aiways ukitokea nchini Brazil.

Ziara hii ilianza tarehe 28 Juni hadi 08 Julai,2019 yenye lengo la kutafuta fursa  za kibiashara, uwekezaji na masoko  kwa bidhaa zinozalishwa Tanzania ukiongozwa na Balozi wa Heshima wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Zanzibar Mhe. Abdulsamad Abdulrahim

The Consulate of Brazil Zanzibar avails itself the assurances of its highest consideration.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.