Baada
ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph
Magufuli, kuagiza sehemu ya Pori la Akiba la Selous kugeuzwa kuwa Hifadhi ya
Taifa ya Nyerere, mchakato wa kutekeleza agizo hili umekamilika. Tarehe 9 Septemba,
2019, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Azimio la Bunge la
kuanzisha Hifadhi ya Taifa ya Nyerere. Tarehe 19 Novemba, 2019, Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, aliweka
sahihi kwenye Tangazo la kuanzisha rasmi Hifadhi ya Taifa ya Nyerere. Kwa
hivyo, Hifadhi ya Taifa ya Nyerere imeanza rasmi tarehe 19 Novemba, 2019.
Hifadhi
ya Taifa ya Nyerere ina ukubwa wa kilometa za mraba 30,893 na kuifanya kuwa
moja ya hifadhi kubwa sana duniani yenye vivutio vingi vya asili na wanyamapori
wengi.
Kadhalika,
kufuatia Azimio la Bunge la tarehe 10 Septemba, 2019 la kuanzisha Hifadhi ya Taifa
ya Kigosi na Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ameweka sahihi matangazo
ya kisheria ya kuanzisha rasmi Hifadhi ya Taifa ya Kigosi na Hifadhi ya Taifa
ya Mto Ugalla. Hifadhi hizi mpya sasa
zinatambuliwa rasmi kisheria kuanzia tarehe 19 Novemba, 2019.
Hifadhi
ya Taifa ya Kigosi ina ukubwa wa kilometa za mraba 7,460. Kadhalika, Hifadhi ya
Taifa ya Mto Ugalla ina ukubwa wa kilomita za mraba 3,865.
Kufuatia
hatua hii, Tanzania sasa inakuwa na jumla ya hifadhi za taifa ishirini na mbili.
Prof. Adolf F. Mkenda
KATIBU MKUU
22 Novemba, 2019
No comments:
Post a Comment