Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein, akiongoza mkutano na Uongozi wa Wizara ya Kilimo Maliasili Uvuvi na Mifugo Zanzibar, wakati wa kuwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango Kazi kwa mwezi wa Julai hadi Disemba 2019/2020, uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar naMwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein ameutaka uongozi wa Wizara ya Kilimo,
Maliasili, Mifugo na Uvuvi kukutana moja kwa moja na wakulima ili kufanikisha dhamira
ya kuwepo matumizi ya mbegu bora za kilimo.
Dk. Shein amesema hayo Ikulu Jijini
Zanzibar, wakati akipokea taarifa ya Utekelezaji wa mpango kazi ya Wizara ya Kilimo,
Maliasili, Mifugo na Uvuvi kwa kipindi cha Julai hadi Disemba 2019/2020.
Alisema pamoja na matumzi ya vyombo vya
Habari vya Redio na Televisheni kuwa na mchango mkubwa katika uhamasishaji wa matumizi
bora ya mbegu za kilimo, ni vyema wataalamu na watendaji wa Wizara hiyo wakakutana
moja kwa moja na wakulima kwa kuzingatia uzito wa jambo hilo.
Alisema uhamasishaji wa matumizi ya mbegu
bora ni jambo zito na linalohitaji kupewa umuhimu na kuwa endelevu ili kuleta matokeo
chanya katika kilimo, hususa nmpunga.
Aidha, ameitaka wizara hiyo kuwa na mipango
mizuri ya mafunzo kwa watendaji wake ili kuondokana na changamoto mbalimbali
,sambamba na kuwa na mipango mbadala katika kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazojitokeza.
Ameeleza ni vyema kukawa na utaratibu maalumu
tekaotekelezwa kwa awamu tofauti kuambatana na ukubwa wa kiwango fedha zitakazopatikana
katika bajeti.
Dk. Shein ameipongeza Wizara hiyo kwa juhudi
za kuwaendeleza kielimu watendaji wake kwa lengo la kukuza uwezo wao, ambapo pia
alitumia fursa hiyo kumpongeza mhitimu wa shahada ya Udaktari (PHD Pathology)kutoka
Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), Ali Mohamed aliehitimu hivi karibuni, hatua
aliyosema itaongeza idadi ya watafiti Wizarani humo.
Rais Dk. Shein aliutaka uongozi wa Wizara
hiyo kuendeleza utamaduni wa kukaa pamoja na uongozi wa Wizara za Fedha na Mipango
pamoja na ile ya Biashara ili kufahamu kwa kina mwenendo wa kibiashara katika masoko
mbalimbali yaliopo nchini ili hatimae kuelewa mahitaji halisi ya aina tofauti za
vyakula.
Vile vile aliutaka uongozi wa Wizara hiyo
kukaa pamoja na watendaji wa Halmashauri za Wilaya na kuangalia namna ya kuwepo
usimamizi mzuri katika uendelezaji wa masoko yaliopo kwa kuwa na mipango borakatikaupangajiwabidhaazao.
Katika hatua nyengine, Dk. Shein ameutaka
uongozi wa Wizara hiyo kutuma waraka Serikalini na kuelezea ukubwa wa changamoto
zinazojitokeza katika ushughulikiaji wa kilimo cha mpunga kinachotegemea mvua,
wakati huu ambapo Serikali imekuwa ikisaidia upatikanaji wa ruzuku na pembejeo mbalimbali
kwa lengo la kuendeleza kilimo hicho.
Alisema kuwepo kwa taarifa za kuchelewa
kuanza kazi za kilimo hicho, kwa madai ya wakulima kuchelewa kutuma fedha za kuchangia
gharama za ukulimaji/kuburuga kwa mategemeo ya fedha hizo kulipwa na Wabunge au
Wawakilishi, hakuendani na azma na dhamira ya Serikali katika uimarishaji wa kilimo
cha mpunga.
Aidha, Dk. Shein aliwataka watendaji wa
Wizara hiyo kuwa wabunifu, waadilifu na kuendelea kufanyakazi kwa misingi ya uzalendo,
sambamba na kujenga mashirikiano ya pamoja kili kupata mafanikio zaidi.
Nae, Katibu Mkuu wa Baraza la
Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Abdulahmid Yahya Mzee aliutaka uongozi wa
Wizara hiyo kuhakikisha kila mara unatowa msukumo na misaada kwa wakulima,
wafugaji na wavuvi nchini kote,ili waweze kupata mafanikio zaidi katika shughuli
zao.
Alisema katika siku za hivi karibuni kumeanzakujitokeza
mizozo kati ya wakulima na wafugaji katika baadhi ya maeneo, hivyo akasisitiza umuhimu
wa kuliangalia suala hilo kwa makini ili kuepusha athari hapo baadae.
Ameupongeza uongozi wa Wizara hiyo kwa
maandalizi na mpangilio bora wa mpango wa Utekelezaji uliowasilishwa, pamoja na
utekelezaji mzuri wa majukumu yao.
Mapema, Waziri wa Kilimo, Maliasili,
Mifugo na Uvuvi,Mmanga Mjengo Mjawiri alisema katika kipindi hicho Wizara hiyo imefanikiwa
kupata mafaniko makubwa katika utekelezaji wa mpango kazi.
Alisema mafanikio hayo yamekuja kutokanana
upatikanaji wa fedha, ambapo jumla ya shilingi Bilioni 12.56 zilipatikana kwa ajili
ya kuendeleza shughuli mbalimbali,ikiwemo za maendeleo.
Aliyataja baadhi ya mafanikio hayo kuwa
ni pamoja na kuanza kwa ujenzi wa Miundombinu ya umwagiliaji maji kwa njia yak
kutumia mabomba katika mabonde saba kupitia mradi ERPP, yakiwemo ya Ole (ekari
9.2), Dobi (ekari 25), Michigini(ekari 28), Kibondemzungu (ekari 25), Koani
(ekari 22), Mchangani (ekari 22) pamoja an Bandamajiekari 15.
Alisema pia ujenzi wa Soko la samaki na
diko la Malindi ulianza pamoja na kufanikiwa kukamilisha ujenzi wa jengo la
hifadhi za TUMCA liliopo Mkokotoni, hifadhi ya CHABAMCA iliopo Mazizini,
sambamba na kukamilika kituo cha ulinzi wa bahari kiliopo kisiwani Pungume.
Alisema ununuzi wa Boti tatu za Doria zenye
thamani ya Dola za Kimarekani 250,000 kutoka Afrika Kusini pamoja na ununuzi wa
boti moja ya uvuvi kutoka nchini Srilanka ulikamilika na hatimae kuwasili
Zanzibar.
Aidha, alisema katika kipindi hicho jumla
ya Wataalii 39,951 (wandani 3,996 na nje 35,955) walitembelea Hifadhi
za Jozani, Masingini, Kiwengwa Pongwe na Ngezi Vumawimbi, huku Hifadhi za Jozani
na Ghubaya Chwaka ikipata tuzo ya Tourism Award kwa kupokea watalii wengi katika
mwaka huo wa 2019.
Vile vile alisema Wizara ilifanikiwa kuendesha
mafunzo ya uchimbaji wa mabwawa na ujengaji wa vizimba vya kufugia majongoo kwa
vijiji vya Uzi, Unguja Ukuu, Fundo pamoja na Pangani, ambapo wafugaji 95 wa majongoo
na samaki walinufaika.
Alieleza kuwa ugawaji wa vifaranga vya
samaki 20,000 ulifanyika katika Shehia za Bumbwini makoba ,Mafufuni, Jozani,
Jadida pamoja na Vifaranga vya majongoo 9,000 kwa shehiya za Uzi, Uzi Ng’ambwa na
Kukuu.
Waziri Mjawiri alisema katika utekelezaji
wa mpango huo pia kulijitokeza baadhi ya changamoto, ikiwemo ya ongezeko la
mvua zaidi ya wastani (milimita 900) jambo lililosababisha mabonde ya mpunga kujaa
maji na kuchelewesha kilimo cha mpunga.
Aidha, alisema wakulima kumi wa Sehiya
ya Chaani walikataa kuchukua fidia za nyumba zao kwa ajili ya kupisha ujenzi wa
miundo mbinu ya umwagiliaji maji (bwawa) kupitia mradi wa kuendeleza miundombinu
ya uwagiliaji maji.
No comments:
Post a Comment