Habari za Punde

Wafanya biashara wanawake kisiwani Pemba wakutana kuwaslilisha katiba

 WAFANYABIASHARA wanawake Kisiwani Pemba, wakiwa katika kikao cha pamoja cha kuwasilisha katiba ya Jumuiya ya wafanyabiashara wanawake Zanzibar, kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Makonyo Wawi mjini Chake Chake.(PICHA NA ABDI SULEIMAN,PEMBA)
 MKUU wa Wilaya ya Micheweni Salama Mbarouk Khatib, akiwasalimia wafanyabiashara wanawake Kisiwnai Pemba, mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mkonyo, kwenye kikao cha kuwasilisha katiba ya jumuiya ya wafanyabiashara wanawake Zanzibar.(PICHA NA ABDI SULEIMAN,PEMBA)
 KATIBU wa Muda wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Wanawake Zanzibar Fatma Mabrouk Khamis akiwasilisha mabadiliko yaliyofanyiwa katiba ya jumuiya hiyo, katika kikao cha pamoja na wafanyabiashara wanawake Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN,PEMBA)
 MWANASHERIA Naima Mwinzagu akiwasilisha baadhi ya vipengele vya sheria ya Jumuiya ya wafanyabiashara wanawake Zanzibar, katika kikao cha pamoja na wafanyabiashara wanawake Kisiwani Pemba huko Makonyo Wawi.(PICHA NA ABDI SULEIMAN,PEMBA)

AFISA Mdhamini Wizara ya Biashara na Viwanda Pemba Ali Suleiman Abeid, akizungumza jambo na baadhi ya wafanyabiashara wanawake wa Pemba, wakati wa kuchagua wajumbe wanne mmoja kutoka kila Wilaya, ambao watawakilisha katika kikao cha bodi ya jumuiya ya wafanyabiashara wanawake Zanzibar.(PICHA NA ABDI SULEIMAN,PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.