Habari za Punde

WAZIRI ANGELLAH KAIRUKI AUPONGEZA MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI WCF

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia uwekezaji Angellah Kairuki (wapili kushoto), akifuatana na Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga (wa kwanza kushoto), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), kwenye viwanja vya Nyakabindi wilayani Bariadi mkoani Simiyu jana. Wapili Kulia ni Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Sebera Fulgence akiwa na Afisa kutoka ofisi ya utawala Neema Mushi. 

Na mwandishi wetu, Simiyu.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki ameupongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kutokana na huduma ambazo imekuwa ikitoa kwa wafanyakazi walioumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi.

Waziri Kairuki ametoa pongezi hizo jana (leo Agosti 3, 2020) wakati alipotembelea katika banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Nyakabindi nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

Waziri Kairuki alitoa pongezi hizo baada ya kupata maelezo ya shughuli za Mfuko yaliyokuwa yakitolewa na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Sebera Fulgence ambapo Waziri alivutiwa na majibu ya namna fidia inavyolipwa kwa mfanyakazi aliyeumia au kufariki kutokana na kazi.

“Mwisho wa siku mtu amepata ulemavu wa kudumu angalau consolation (faraja) anayopata ni kuona wanae wanaendelea vizuri au kama amefariki walau fidia isaidie watoto na mjane pia, lengo la serikali ni ku- support for real, ninawapongeza sana kwa kazi nzuri mnayofanya.” Alisema Waziri Kairuki ambaye alikuwa amefuatana na Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga.

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi unashiriki katika maonesho hayo ili kukutana na wadau wote na wananchi kwa ujumla wakiwemo wafanyakazi kutoka sekta ya Umma na Binafsi

Kauli mbiu ya mwaka huu ya maonesho hayo yanayofanyika mkoani Simiyu kwa mwaka wa tatu mfululizo ni “Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua Viongozi Bora 2020.”.

 Afisa kutoka ofisi ya utawala WCF, Neema Mushi.
 Wananchi wakipata maelezo kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi kwenye banda la WCF viwanja vya Nyakabindi.
Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Sebera Fulgence (kulia), akimfafanulia jambo mfanyakazi huyu aliyetembelea banda la WCF viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu Agosti 3, 2020.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.