Habari za Punde

Makabidhiano ya Idara ya Nyaraka na Kumbukumbu


. Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe Lela Muhamed Mussa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman wakisaini vitabu vya kumbukumbu ya makabidhiano ya majukumu ya kiutendaji 

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe Lela Muhamed Mussa akimkabidhi nyaraka muhimu  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman .

Na RAYA HAMAD  (OR- KSUUB)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman amekabidhiwa  Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu  na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe Lela Muhamed Mussa .

Mara baada ya makabidhianao hayo Waziri Haroun amewaasa wafanyakazi kuwa waadilifu kwani nyaraka zina thamani kubwa  na kuahidi kuimarisha zaidi taasisi hio hasa katika masuala ya kuweka kumbukumbu kwani ni hazina muhimu kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na kuhakikisha wafanyakazi wanapaiwta mafunzo mbalimbali pamoja na stahiki zao

Mhe Haroun  amezuwia  kwa muda  makubaliano yote yaliyoihusisha Taasisi ya Nyaraka na kumbukumbu ili kujiridhisha juu ya utaratibu uliotumika  ameahidi kuimarisha mashirikiano na wote wenye nia njema ya kuisaidia  Zanzibar kwa njia ambazo ni za kheri isiwe makubaliano ya kunufaisha upande mmoja  ila yawe  yanazinanufaika pande zote  kwa maslahi ya taifa

‘Kuna nyaraka zilizowahi kuibiwa na waliotoa ni wafanyakazi kutoka taasisi hii Serikali ikachukuwa hatua kwa wale waliohusika lakini nasikitishwa sana kuona kumbe maradhi haya hayajesha ‘

Aidha Mhe Haroun amekemea tabia na mtindo uliozuka hivi sasa kwa baadhi ya wafanyakazi na watendaji wa Serikali wasiowaaminifu kutoa siri za Serikali na kuzisambaza kupitia magurupu mbali mbali ya mitandao ya kijamii jambo ambalo ni kinyume na maadili na taratibu za kiutumishi 

‘ kuanzia sasa mfanyakazi yeyote wa Serikali tukimbaini na akijulikana anatoa siri za Serikali hatua kali za kisheria zitachukuliwa naomba wafanyakazi na watendaji waelewe kuwa  tunafatilia kwa makini sana wale wote wanaovujisha siri za Serikali na baadhi yao tayari tumeshawapata na watachukuliwa hatuwa za kinidhamu’ alilisitiza 

Nae Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mhe Lela Muhamed Mussa amesema nyaraka ni rasilimali muhimu na inayohitaji kuangaliwa kwa umakini sana katika kipindi cha miaka mitano  ambapo amemuomba Waziri Haroun kuangalia  makubaliano yaliyofikiwa kati ya Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu ya Zanzibar na Taasisi nyengine zilizoingia makubaliano hayo

Mhe Lela amekabidhi taarifa  ya utendaji kwa kipindi cha miaka mitano, muundo wa taasisi  na vitengo mbalimbali,  nakala za baadhi ya nyaraka zilizowahi kuibiwa na kupatikana kutoka nchi mbali mbali pamoja na nyaraka za makubaliano yaliyofikiwa na Taasisi hio

Aidha Mhe Lela amemkabidhi  Waziri Haroun Mkataba wa makubaliano ya awali baina ya Idara ya Nyaraka na Makumbusho ya Zanzibar na Makumbusho ya Taifa na Nyaraka ya Oman yaliyosainiwa Tarehe 30 April, 2020

Makubaliano ya Makabidhiano ya Uhamishaji wa nyaraka baina ya Wizara ya Habari Utalii na  Mambo ya kale na Bi Saada Shaaban Shahdad, Nyaraka ya fotokopi ya andiko binafsi la Mhe Salim Bin Nasser Al-Ismail ambayo ameiwasilisha Idara ya Makumbusho na Nyaraka Zanzibar kwa madhumuni ya kuhifadhiwa  

Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu za Serikali ndio yenye dhamana ya kuzihifadhi na kuzitunza nyaraka zote katika eneo salama  hivyo nyaraka zinazohusiana na  maandishi zitaendelea kuwa katika Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora na yale yanayohusiana na mambo ya  kale yakiwemo makumbusho yataendelea kubakia kwa Wizara husika  ambayo ni Wizara ya  Utalii Mambo ya kale

Makabidhiano hayo yalihudhuriwa na viongozi mbali mbali kutoka  Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi na Utawala Bora, Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale na wafanyakazi wa Taasisi ya Nyaraka na Kumbukumbu katika ukumbi wa taasisi hio Kilimani

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.