STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS
SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar Januari 03, 202i
WAZIRI wa Nchi (OR) Afisi ya Rais, Katiba,
Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman, amesema Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka mikakati maalum kwa kipindi cha mwaka 2017 –
2022 ikiwa ni hatua ya kupambana na
vitendo vya Udhalilishaji dhidi ya watoto na wanawake nchini.
Waziri Haroun amesema hayo wakati akifungua Tamasha la kwanza
la pongezi kwa Wana Sunni Madrasa katika
hafla iliyofanyika Ukumbi wa Sunni Madrasa, Mkunazini jijini Zanzibar.
Akimuwakilisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi; Waziri Haroun aliahidi kukutana na wadau
wanaoshughulikia vitendo vya Udhalilishaji, ikiwemo Jeshi la Polisi, Mahakama
na Ofisi ya Muendesha Mashtaka kwa lengo
la kujenga mikakati ili kuharakisha
usikilizaji wa kesi za makosa hayo
yalioshamiri nchini.
Alisema Serikali hairidhishwi na mlundikano uliopo wa kesi za
udhalilishaji na hivyo akaitaka jamii
kujenga mashirikiano na vyombo vya sheria ili kufanikisha mchakato wa kesi
pamoja na kuondokana na muhali.
Alitumia fursa hiyo kuwapongeza walimu wanaofundisha fani hiyo
ya ‘Nasheed’ kwa kazi nzuri wanayofanya pamoja
na kuwoamba kuendelea na juhudi
za kuisambaza taaluma hiyo hadi vijijini Unguja na Pemba.
Katika hafla hiyo Waziri Haroun alikabidhi zawadi kwa washindi
wa Tamasha hilo la ‘Nasheed’ , ambapo mwanafunzi Nasra Abdalla Mohamed alikuwa
mshindi wa kwanza na hivyo kuzawadiwa Friji, Mkoba pamoja na Ma-shafu.
Aidha mwanafunzi Asiat Ramadhan Jussa alikuwa mshindi wa pili
na kuzawadiwa zawadi za Cherehani, Mkoba
na Mas-hafu, huku mwanafunzi Mudrik Msellem Ali akiondoka na ushindi wa tatu na
kuzawadiwa Baiskeli, Mkoba na Mas-hafu.
Mapema, Katibu mtendaji Idara
ya Sensa na Sanaa Omar Abdalla
Adamu aliwashukuru waandaji wa Tamasha hilo na kusema wamekamilisha taratibu
zote za kisheria na kufauta mila, silka na utamaduni wa Mzanzibari.
Nae, Sheikh Habibu Othman ‘Mazinge’ aliwata waislamu nchini
kote kumuomba Mwenyezi Mungu adumishe
amani na umoja miongoni mwa Wazanzibari.
Aidha, aliumuomba Mwenyezi Mungu kuilinda Zanzibar ili
iendelee kubaki na amani na usalama
pamoja na kuwajaalia viongozi wote wa Serikali amani.
Katika tamasha hilo wanafunzi 20 walisoma ‘Nasheed’ mbali
mbali zenye maudhui ya kupinga vitendo vya Udhalilishaji kwa watoto na
wanawake.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982.
Fax: 024 2231822
E-mail:
abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment