Habari za Punde

NMB Yachukua Nafasi ya Tatu Kwa Ulipaji wa Kodi kwa Hiari Nchini.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi Cheti cha Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi. Ruth Zaipuna, Mchango wake Mkubwa katika Ulipaji wa Kodi kwa Hiari na Kutunukiwa Cheti cha Pongezi cha Msindi wa Tatu Tanzania, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji Kiuchumi likiwa sambamba na Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.(iliyokuwa Tanganyika) Kongamano hilo limefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Jijini Zanzibar.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi.Ruth Zaipuna akifurahia jambo wakati akikabidhiwa Cheti cha Pongezi  cha Ulipaji Kodi kwa Hiari na kushika nafasi ya Tatu Tanzania, akikabidhiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji Kiuchumi Nchini Kuadhimisha Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara(iliyokuwa Tanganyika) hafla hiyo iliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika viwanja vya Hoteli ya Golden Tulip Jirani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Mustafa Idrisa Kitwana.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Bi, Ruth Zaipuna akisoma Jirida  kabla ya kuaza kwa Kongamano la Uwekezaji Kiuchumi  Kuadhimisha Miaka 60 ua Uhuru, kabla ya kufunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Jirani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.
Washiriki wa Kongamano la Uwekezaji Kiuchumi kutoka Tanzania na Nje ya Tanzania wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akilifungua Kongamano hilo likienda sambamba na Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara(iliyokuwa Tanganyika) (hayupo pichani) ufunguzi huo umefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip jirani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

Maofisa wa Benki ya NMB wakifuatilia ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji Kiuchumi Tanzania wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia na kulifungua katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip jirani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, ikiwa sambambana na kuelekele Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Uwekezaji Kiuchumi Nchini likienda sambamba na Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.(iliyokuwa Tanganyika) Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip jirani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar, na kuhudhuriwa na Wawekezaji kuta Nje ya Nchi na Tanzania.


 



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.