Habari za Punde

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Lela Azungumza na Wanafunzi Waliorejea Shuleni na Wanaojiandaa Mitihani ya Darasa la Nne na la Saba

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Lela Muhammed Mussa akiwasalimia Wanafunzi wakati wa ziara yake kutembelea Skuli za Mkoa wa Kaskazini Unguja na kuzungumza na Wanafunzi waliuorejea Skuli na Wanaojiandaa na Mitihani ya Darasa la Nne na la Saba.

Waziri wa Elimu na  Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Muhamed Mussa amefanya ziara ya kutembelea Wanafunzi ambao wamerejea skuli  baaada ya kuacha masomo  kutokana na  sababu mbalimbali za kimaisha na  kifamilia katika Mkoa wa kaskazini Unguja.

Katika ziara hiyo Waziri Mhe.lela  alipata fursa ya kukagua ujenzi wa madarasa ya Elimu mbadala pamoja na  kuzungumza na wanafunzi ambao wanajitarisha kufanya mitihani ya Taifa ya darasa la nne na saba katika skuli ya Bububu ambapo aliwata kusoma kwa bidii ili kuweza kujitarisha na mitihani yao  ambayo inatarajiaa kuanza mapema wiki ijayo.

Aidha amewataka Walimu Wakuu kuwasimamia pamoja na wasimamizi wa mitihani kuwa waadilifu na  kujiepusha na vindendo vyovyote ambayo vitapelekea kuleta taharuki wakati zoezi la ufanyaji mitihani likiendelea.






No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.