Habari za Punde

Waziri wa Fedha na Mipango Tanzania Dkt.Nchemba Akutana na Mkurugenzi wa AfDB

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeiwakilisha Tanzania kwenye Benki hiyo, Bw. Jonathan Nzayikorera, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, kwa ziara ya kikazi ya siku nne.

Na Ramadhani Kisimba, WFM, Dar es Salaam

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) anayeiwakilisha Tanzania kwenye Benki hiyo, Bw. Jonathan Nzayikorera.

 

Dkt. Nchemba amekutana na Mkurugenzi huyo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaamakiwa safarini kuelekea Bujumbura nchini Burundi, kuhudhuria Mkutano wa 43 wa Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Masharikiutakaofanyika tarehe 23 Februari, 2023.

 

Bw. Nzayikorera amewasili nchini leo tarehe 21 Februari, 2023 kwa ziara ya kikazi ya siku nneambapo pamoja na mambo mengine atakagua maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika.

 

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeiwakilisha Tanzania kwenye Benki hiyo, Bw. Jonathan Nzayikorera, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, kwa ziara ya kikazi ya siku nne.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.