Habari za Punde

Balozi Mdogo wa China Zanzibar Atimiza Ahadi yake kwa Taasisi za Zanzibar Maisha Bora Foundation Kukabidhi Mikoba ya Skuli

 

MWENYEKITI wa Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akikabidhiwa Mikoba 100 ya Skuli na Balozi Mdogo wa China anayefanyia Kazi zake Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng ikiwa ni ahadi yake aliyoitowa wakati wa Maadhimisho ya mwaka mmoja wa Taasisi hiyo (ZMBF) hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi za (ZMBF) migombani Wilaya ya Mjini Unguja leo 28-3-2023

MWENYEKITI wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi akizungumza na Balozi Mdogo wa China anayefanyia Kazi zake Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng, alipofika katika Ofisi za (ZMBF) migombani kwa mazungumzo na kukabidhi mikoba 100 ya Skuli ikiwa ni ahadi yake aliyoitowa wakati wa maadhimisho ya mwaka mmoja wa (ZMBF) hafla hiyo iliyofanyika leo 28-3-2023 katika ofisi za taasisi hiyo migombani Wilaya ya Mjini Unguja

Mwenyekiti wa Bodi ya taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) ambae pia ni Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mariam Mwinyi alisema Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni mwezi wa kutoa sana na kuwapa wanaohitaji.

Mama Mariam ameyasema hayo ofisini kwake Migombani, Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mijini Magharibi, wakati akipokea zawadi ya mikoba 100 ya skuli kutoka kwa Balozi Mdogo wa China aliepo Zanzibar, Zhang Zhisheng ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa Machi 20, mwaka huu katika halfa ya kutimiza mwaka mmoja wa taasisi ya “Zanzibar Maisha Bora Foundation” kwenye ukumbi wa Golden, Tulip, Uwanja wa ndege, Zanzibar.

Alisema zawadi hizo zimekuja muda sahihi kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ambacho ni kizuri kutoa na kuwapa wanaohitaji, hivyo aliahidi mikoba hiyo kuwapatia wanafunzi wa skuli mbali mbali za Zanzibar.

Mama Mariam ambae pia ni Mwanzilishi na Msarifu wa (ZMBF) alitumia fursa hiyo kuushukuru ubalozi mdogo wa China kwa kutekeleza ahadi yao kivitendo kwa ZMBF pia kuendeleza ushirikiano wa kirafiki uliopo kwa taasisi hiyo.

Alieleza Ubalozi Mdogo wa China umeisaidia sana ZMBF hata kabla ya kukamilisha mwaka mmoja tokea kuasisiwa kwake mwaka 2021 na kuzinduliwa mwaka 2022 na kueleza furaha yake kuona ubalozi huo unafuatia kwa karibu harakati za maendeleo zinazofanywa na ZMBF za kuisaidia jamii na Wazanzibar kwa ujumla.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Balozi mdogo wa China, Zhang Zhisheng alisema anaamini zawadi hiyo itawafaa na kufurahiwa na watoto wadogo wa shule.

Balozi Zhisheng alisema, China na Zanzibar zimekua na ushirikiano wa kirafiki kwa muda mrefu na kwamba uhusiano wao haukuishia tu kwa Serikali za Tanzania lakini kwa wa watu wa nchi za pande mbili hizo ikiweo pia na taasisi binafsi zenye nia ya kuendeleza malengo ya Serikali ikiwemo maendeleo kwa watu wao.

Alisema ubalozi mdogo wa China kwa kushirikiana na Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation wamekua wakifanyakazi bega kwa beka katika hatua za kuunga mkono maendeleo yanayofanywa na Serikali ya Mapindizi ya Zanzibar kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Hata hivyo, ubalozi huo umeahidi kuendelea kuiungamkono Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar hata asasi za kiraia zinazoiungamkono serikali katika kuwaletea maendeleo watu wao.

Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation iliasisiwa tangu mwaka 2021 na kuzinduliwa mwaka 2022 ambapo mwezi Februari mwaka huu ilitimiza mwaka mmoja tokea kuasisiwa na sasa inatekeleza mpango mkakati wa miaka mitatu 2023 hadi 2025 ambao unatarajia kutumia dola za Marekani milioni mbili ili kufanikisha malengo iliyojiwekea.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.