Mkoa wa Kusini Pemba
Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Msoud Othman, amesema athari zinazotokana na uharibifu wa
mazingira Zanzibar ni kubwa na kwamba ni
lazima wananchi , viongozi na taasisi mbali mbali kuungana na kuwa na utamaduni
wa kupanda miti na kuithamini ili kulikabili janga hilo.
Mhe. Othman
ameyasema hayo kwa nyakati tofauti katika mkutano wake na Viongozi , masheha na wafanyakazi wa
Mabaraza ya Mji wa Chake na Mkoani Mkoa
wa Kusini Pemba akiwa katika ziara ya kikazi mkoani humo.
Mhe. Othman
alikuwa akielekeza kuhusu na hali halisi ya uharibufu wa mazingira Zanzibar
pamoja na haja ya viongozi na wananchi kushirikiana pamoja katika utekelezaji
wa mpango wa Serikali wa wa urithi wa Kijani Zanibar unaotarajiwa kutekelezwa
hivi karibuni wenye lengo la kutunza,
kulinda na kuhifadhi mazingira ya Zanzibar.
Amewataka
viongozi hao pamoja na wananchi kufahamu kwamba mpango huo unaotarajiwa
kutekelezwa ni wa kitaifa ambao unatarajiwa kuisaidia sana Zanzibar kulinda na
kuhifadhi mazingira yake ili kujikinga na majanga yatokanayo na athari za
mabadiliko ya tabia nchi na binaadamu.
Mhe. Makamu
amewaeleza viongozi hao na wananchi kuwa changamoto iliyopo ya athari ya kimazinmgira Zanzibar
inaendelea kuwa kubwa na iwapo hatua za pamoja hazitachukuliwa inaweza kuleata
maafa ya ,kijamii na kiuchumi hapa Zanzibar.
Amesema
kwamba hali ya uchafuzi na uharibifu wa mazingira tayari imechangia miti mingi
ya asili ambayo ni ya matunda kuanza kupotea na kwamba kizazi kijacho
hakitaweza kufaidika na rasilimazili zilizokuwepo ambazo wazazi wao wamechangia
kuziharibu na kuzipoteza.
Aamesema
mbali na uharibu huo wa mazingira pia
kasi ya ukaji wa watu halingani na hali uhifadhi wa mazingira ikiwemo
kuchafuliwa na kupotea vyanzo vya maji
na hivyo wananchi kukosa huduma muhimu ya maji.
Amesema
kwamba hivi sasa maeneo mengi ya Zanzinbar maji yameanza kupotea na kwamba
visima vingi vya maji safi na salama vilazimika kuchimbwa kwa kina kirefu kwa
kuwa maji yamepotea kutokana na kuharibika kwa mazingira.
Mhe. Othman
amefahamisha kwamba hata eneo la kilimo a mbalo ni ukanda wa maghareibi ya
visiwa vya unguja na pemba tayari limeatjhriwa na hali hiyo kwa kuendeleza
shughuli za kibaadamu ukiwemo ujenzi wa nyumba za makaazi.
Amewataka
viongozi wanaosimamia serikali za Mitaa kuhakikisha kwamba nazingatia na
kusimamia ipasavyo sheria na taratibu za mipango miji ili Zanzibar isiendelee
kuathariwa na matatizo ya kimazingira na
kuweza kuwarithisha vizazi vijavyo mazingira bora na salama.
Amewataka
viongozi hao na wananchi kushirikiana na taasisi mbali mbali ili kuanza
kujipanga kwa kuyain isha maeneo yanayohitaji kupandwa miti ya namna tofauti
kulingana na uasili wa miti iliyokuwepo kwenye maeneo hayo.
Naye Mkuu
wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Matar Zahor Masoud amesema kwamba mbali na
kuipokea Mpango wa serikali kuu kuhusu
kuirejesha Zanzibar kuwa ya kijani lakini katika ngazi za halimashauri na mikoa
tayari wameandaa miakakatgi mbali mbali itayaoungana na mpango huo katika
kulikabili suala la mazingira.
Amesema
kwamba katika mpangowa wao wanakusudia kuwashirikisha na kuwarkithisha
wanafunzi kutoka ngazi za awali juu ya
kupanda na kuhifadhi miti katika maeneo ya
skuli zao katika kipindi chote cha wanafunzi kuwepo kwao maskulini.
Nao
wakurugenzi wa Mabaraza ya Miji ya Chake Ndugu Maulid Mwalimu Ali na wa Mkoani Ndugu Yussuf Kaiza
Makame wakiwasilisha ripoti ya utekelizaji wa shughuli za mabaraza hayo kwa
kipindi cha nusu mwaka wamesema kwamba
shughuli nyingi licha ya kuwepo kwa changamoto mbali mbali, lakini wamefanikiwa
kuzitekeleza kwa ufanisi mkubwa.
Mwisho
No comments:
Post a Comment