Habari za Punde

Serikali yaanza kuwanoa wakaguzi wa ndani



Joseph Ngilisho, Arusha
SERIKALI imeanza kutekeleza mpango  wa kuwajengea uwezo wakaguzi wa ndani wa umma ili waweze kushiriki kikamilifu katika mabadiliko baada ya kuridhia mwongozo wa viwango vya kimataifa uliotolewa mwaka 2011.

Kauli hiyo imetolewa  jana  na Mkaguzi Mkuu wa ndani wa serikali , Mohamed Mtonga wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa wakaguzi wa ndani wa serikali kanda ya kaskazini.

 Alisema mkutano huo unalenga kuwajengea uwezo wakaguzi wa ndani jinsi ya kuandaa miongozo inayoendana na maadili ya shughuli zao huku ikizingatia viwango vya ukaguzi wa kimataifa.

Mtonga alisema katika kuridhia mpango huo wa  ukaguzi wa ndani katika sekta ya umma ni lazima uzingatie  viwango vya kimataifa ili kuongeza uwajibikaji katika sekta ya umma.


“Ili kuhakikisha ukaguzi huo unaendana na viwango vya kimataifa lazima kutayarishwe mfumo maalumu wa uhakiki wa ubora wa ukaguzi wa ndani  ambapo swala la maadili na uwajibikaji wa wakaguzi wa ndani litapewa uzito wa kutosha katika mfumo huo mpya nah ii ndio njia pekee itakayowezesha kuboresha shughuli zao,” alisema Mtonga.

Alisema wanataka wakaguzi wa ndani kufanya  shughuli zao kwa uhuru zaidi bila kuingiliwa na mtu yeyote na hatimaye kuweza kuleta taarifa sahihi kuhusiana na  ukaguzi wao.

Alifafanua zaidi kuwa, baada ya mafunzo hayo wakaguzi wa ndani wataweza kutoa huduma kwa viwango vinavyotakiwa huku wakifanya kazi zao kwa kufuata maadili na miongozo waliyopewa na hiyo itawezesha kuboresha utendaji kazi wao kwa ujumla.

Mafunzo hayo ya siku tatu  ya  wakaguzi wa ndani wa umma kanda ya kaskazini ni ya pili kufanyika ambapo lengo la serikali ni kuendesha mafunzo kama hayo katika kanda zote nchini.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.