Na Mwandishi wetu, Pwani
WATU
wanane wakiwemo wanafunzi wanne wa shule ya sekondari Msolwa wamekufa baada ya
magari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na fuso katika eneo la
Kibiki tarafa ya Chalinze mkoani Pwani.
Ajali hiyo iliyotokea saa 12 :20 jioni iliyahusisha
magari yenye namba za usajili T.363 AZG,
Toyota mark II lililokuwa likiendeshwa na
Abuu Ahmedi (21) na fuso lenye
namba za usajili T.433 AYQ lililokuwa likiendeshwa na Mweta Daniel (40).
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani,Gregory Mushi alisema chanzo cha ajali hiyo ni baada ya
dereva wa fuso kushindwa kulidhibiti gari lake na kupoteza mwelekeo kisha
kuligonga gari dogo.
Kamanda Mushi aliwataja watu waliokufa katika ajali hiyo
kuwa ni Esau Enos (16) ambae ni mwanafunzi
wa kidato cha tatu, Bahati George (18), mwanafunzi wa kidato cha nne,Latifa
Maneno Shabani (17), mwanafunzi wa kidato cha nne,Stela Issack Kazimoto (18)
wanafunzi wa kidato cha tatu na Hassani Kulunga ambae umri wake bado haujafahamika.
Wengine
ni Maria Sadiki Lelela, Samwel Ismail, miaka 3 – 4 na Abuu Ahmed (21) ambaye alikuwa dereva wa gari
dogo.
Aidha alisema ajali hiyo ilisababisha majeraha kwa abiria
waliokuwa katika fuso ambao ni William
Tobias (30) na Ahmada Ahmada Juma (36), aliyekuwa utingo wa fuso hilo na wanaendelea
na matibabu katika kituo cha afya Chalinze na miili ya marehemu imehifadhiwa hospitali
ya teule ya Tumbi Kibaha.
Kamanda Mushi alitoa wito kwa madereva kuzingatia sheria
za usalama barabarani ili kuepuka ajali za kizembe.
No comments:
Post a Comment