Na Masanja Mabula, Pemba
BAADHI ya wanachama wa Jumuiya ya Watu
wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Kisiwani Pemba wamedaiwa kuendelea kueneza
virusi vya Ukimwi kwa makusudi licha ya kujitambua kuwa wanaishi na maambukizi
ya ugonjwa huo, hali iliyowapa hofu kubwa wananchi.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi Wete, Katibu wa Jumuiya ya Watu wanaoishi na Virusi
vya Ukimwi Zanzibar, Saade Said Saduni alisema hali hiyo inakwamisha
kufanikisha lengo la serikali la kupunguza maambukizi mapya katika jamii.
Alisema
jumuiya hiyo kisiwani Pemba imepokea
taarifa hizo kutoka kwa wananchi na kwamba wanaendelea kuzifanyia kazi na
kuongeza kwamba upelelezi wa awali umeonyesha kuwepo uenezaji wa virusi hivyo
kwa makusudi kunakofanywa na wanachama wa jumuiya hiyo.
"Taarifa
hizi tunazo na tunazifanyia kazi , kwani tumezipokea kutoka kwa wananchi na
baada ya kufanya ufuatiliaji wa awali tumebaini kuwepo na ukweli ndani yake,
lakini wacha tuendelee kufanya uchunguzi zaidi, " alifahamisha.
Aidha
Saade amefahamisha jumuiya hiyo haiwezi kuvifumbia macho vitendo hivyo ambavyo
vinaweza kuleta athari zaidi kwa jamii kutokana na kwamba maambukizi mapya
yanaweza kuongezeka.
Katika
hatua nyingine Saade amewataka viongozi kuanzia ngazi za shina hadi taifa
kuendelea kushirikiana na ZPHA+ katika kutoa elimu kwa jamii ili kuona kwamba
elimu hiyo inaleta faida kwa wanajamii.
Alieleza kwamba kwa sasa ushirikiano kutoka kwa
viongozi hao haupatikani kutokana na viongozi hao kushindwa kuendelea kutoa
elimu ya Ukimwi baada ya wafadhili waliokuwa wakifadhili kamati za ukimwi
kusitisha misaada yao.
No comments:
Post a Comment