Na
Mwashamba Juma
MBUZI
74 walikumbwa na maradhi ya baridi katika kijiji cha Matemwe Mkoa wa Kaskazini
Unguja katika kipindi cha kuanzia mwezi
Disemba mwaka jana na Januari mwaka huu,
ambapo kati yao
mbuzi 31 walikufa.
Mkurugenzi
Idara ya huduma za utabibu wa mifugo Zanzibar, Dk. Yussuf Haji Khamis, alisema
mwezi Disemba mbuzi 54 waliugua ugonjwa huo na mbuzi 17 walifariki.
Alisema
kwa mwezi Januari mbuzi 20 waliugua, ambapo mbuzi 14 walikufa.
Mkurugenzi
huyo alisema tayari wametuma timu ya madaktari bingwa wa mifugo katika Wilaya
ya Kaskazi hasa katika maeneo ya Matemwe, Pwani Mchangani na vijiji jirani
kwenda kufanya uchunguzi wa kina.
Aliwataka
wafugaji wilayani humo kujenga mabanda kwa ajili mifugo yao
ili kuwanusuru na maradhi pamoja na kuwataka kuvitumia vituo vya afya hasa wanapogundua matatizo ya mifugo yao.
Kuhusu
taarifa za kuwepo maradhi ya nyimonia ambayo kitaalamu yanajulikana kama Contagious
Caprine Pleuro Pneumonia (CCPP), Mkurugenzi huyo alisema bado hawajathibitisha
kuwepo maradhi hayo
Kwa
mujibu wa utafiti mgodo walioufanya mara baada ya kupokea taarifa za kuwepo kwa
maradhi hayo, Dk. Yussuf alisema waliamua kuchukua mbuzi aliekufa na kumfanyia
uchunguzi kupitia mapafu, figo, damu, maini na kinyesi, chake, na kubaini kuwa
baridi kali iliyopo katika maeneo wanaofugwa mbuzi hao ndio chazo cha mbuzi hao
kufa.
“Tatizo
la wafugaji wa Matemwe hawajengi mabanda kwa ajili ya mifugo yao ukiangalia
wapo karibu na ukanda wa bahari, hivyo mwanyama wengi wanaathiriwa na baridi
kali hasa nyakati za usiku hali inayowasababishia wanyama hao kuugua mara kwa
mara,” alisema Mkurugezi huyo.
Dk.
Yussuf pia alipinga kuwepo kwa taarifa za watu kula mizoga na kusema kuwa
Wizara yake haijapokea wala kuwa na taarifa hizo.
No comments:
Post a Comment