Na Masanja Mabula,Pemba,
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mwanaidi
Saleh, amewataka walimu kuwa wastahamilivu wakati serikali inajiandaa kufanya
marekebisho ya mishahara kwa kuzingatia mpango kazi.
Alisema mpango huo utawawezesha walimu walioajiriwa miaka ya 1970
wenye vyeti kunufaika na mabadiliko
hayo hali ambayo itaondoa malalamiko ya
muda mrefu ambayo yamekuwa yakitolewa na
kuhusiana na mpango huo.
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na walimu wakuu wa skuli za
maandalizi , msingi na sekondari wa mkoa wa kaskazini Pemba
kwenye ukumbi wa Jamhuri Wete.
Aliema wakati wizara ikijiandaa kufanya marekebisho hayo, ni vyema
walimu wakuu mkoa huo kusimamia vizuri
nidhamu kwa walimu ili kuwafanya waweze kutimiza majukumu ya kazi zao kwa
ufanisi.
“Ni jukumu lenu walimu wakuu kuhakikisha walimu katika skuli zenu
wanakuwa na nidhamu ya kazi ikiwa ni pamoja na kuandaa mpango kazi kwa ajili ya
wanafunzi kila siku,”alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Utumishi wa wizara hiyo, Vuai Khamis
Juma, aliwasisitiza walimu wakuu kuwasimamia vijana wanaoajiriwa ili waweze
kujaza vyema mikataba yao .
Alisema wizara inatambua kuwepo na udanganyifu unaofanywa na baadhi ya
walimu juu ya tarehe zao za kuzaliwa.
Nao walimu wakuu wakichangia kwenye kikao hicho walihoji tafiti
zilizotumika kubadilisha mitaala ya elimu kwa wafaunzi na kuongeza kwamba
mwanafunzi wa darasa la kwanza kubebesha mzingo wa masomo nane ni vigumu
kuyamudu.
Walisema ni vyema wizara hiyo
ikawapunguzia masomo wanafunzi hao ili waweze kuwa na uwelewa wa kutosha.
Hahahahaa! ni joke ya mwaka. Wacha joke Waziri. Unasema mpango utawasaidia pia waalimu walioajiriwa miaka ya 1970? Huachi wewe! Kama mwalimu aliajiriwa mwaka 1970 na alipoajiriwa alikuwa na miaka 20 sasa ana miaka 64. Kwani kisheria anatakiwa kustaafu akiwa na umri gani. Jee mpango huo utakwenda kumsaidia kaburini? Mimi naona wapangie mafao mazuri ya kustaafu ili waondoke na donge nono makamalizie maisha yao baada ya kuitumika wizara kwa mika yote hiyo ya kujenga utu wa watu! Usitanie mheshiwa! Hiyo sio kuwatuliza ,hiyo ni kuwachanganya katika kufiria retirement age.
ReplyDelete