Na
Abdulla Ali na Rahma Khamis - Maelezo
Kifafa
cha Mimba ni miongoni mwa mambo matano makuu yanayosababisha vifo vya moja kwa
moja vya akina mama wajawazito Nchini.
Hayo
yameelezwa na Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mahamoud Thabit Kombo wakati
akijibu swali la mwakilishi wa nafasi za wanawake Mhe. Shadya Mohammed Suleiman
katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar
aliyetaka kujua ni vipi wizara ya afya Zanzibar imejipanga kukabiliana na
tatizo la vifo vya akina mama wajawazito vinavyotokea wakati wa kujifungua.
Amesema
kuwa miongoni mwa mambo yanayosababisha vifo vya moja kwa moja vya akina mama
ni pamoja na Kutokwa na damu nyingi kabla au baada ya kujifungua (Haemorrage), Shindikizo
la damu wakati wa ujauzito (Hypertensive Disorder During Pregnancy), Uzazi kanadamizi
(Obstructed Labour), Maambukizo kwenye mfumo mzima wa damu (Sepsis) ambavyo
hupelekea kuharibika au utoaji wa mimba usio salama unaopelekea unaopelekea
maambukizi kwenye mfumo mzima wa damu (Septic Abortion).
Amefahamisha
kuwa Serikali kupitia Wizara yake imekuwa ikiwashajihisha sana akina mama kuanza
kwenda vituo vya afya mapema kwa ajili ya kupima ujauzito ambapo mama mjamzito
anatakiwa kuhudhuria kituo cha afya kila baada ya wiki 2 hadi Mwezi 1.
Ametanabahisha
kuwa iwapo akina mama watakwenda vituo vya afya mapema itawapelekea kuvifahamu
viashiario hatari kwa wakati ambavyo vitaweza kushughulikiwa na kutafutiwa
ufumbuzi kwa muda muwafaka kama miongozo ya huduma ya dharura kwa akina mama na
watoto wachanga inavyoeleza.
Hata
hivyo Naibu huyo amewataka akina mama wajawazito kuhudhuria vituo vya afya
mapema na kwa mpangilio maalum unaoshauriwa na wataalamu wa afya kwani
kutasaidia kupunguza matatizo ya vifo kwa akina mama hao wakati na baada ya
kujifungua.
Sambamba
na hayo amesema Wizara yake inajitahidi kuongeza wafanyakazi katika vituo vya
afya mbalimbali vilivyopo Nchini hususan Vijijini kwa mujibu wa hali ya
kiuchumi itakavyoruhusu.
IMETOLEWA
NA HABARI MAELEZO- ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment